JamiiForums
June 10, 2025 at 06:49 PM
KENYA: Matokeo ya Uchunguzi wa Daktari yanapingana na ripoti ya Polisi iliyosema kuwa Mwanaharakati na Mwanamitandao, Albert Ojwang' alifariki kwa kujigonga Kichwa kwenye ukuta wa chumba cha Mahabusu katika Kituo Kikuu cha Polisi, alipokuwa akishikiliwa kwa tuhuma za kuchapisha maandiko yaliyolenga kumchafua Naibu Mkuu wa Polisi
Daktari wa Serikali, Bernard Midia, amesema kama Ojwang’ angejigonga ukutani, Damu ingetoka mbele ya Kichwa, lakini walikuta michubuko mbalimbali Kichwani, Usoni, pembeni na nyuma ya Kichwa, ikionesha kuwa majeraha hayo hakuweza kujisababishia mwenyewe
Midia, ambaye alifanya uchunguzi huo pamoja na mwakilishi wa Familia, Mutuma Zambezi, alikanusha uwezekano wa Ojwang' kujijeruhi. Alisema, "Tunapojumuisha pamoja na majeraha mengine yaliyosambaa sehemu mbalimbali za Mwili, ikiwemo Mikononi na Kiwiliwili, basi hii haiwezekani kuwa ni jeraha alilojifanyia mwenyewe
Soma https://jamii.app/PostmortemResults
😢
👍
😂
❤️
🙏
🇹🇿
😮
❤
💔
📼
48