
JamiiForums
June 11, 2025 at 11:38 AM
Aliyekuwa Jaji Mkuu wa Kenya, Dkt. Willy Mutunga, Wakili Mwandamizi Martha Karua, pamoja na watu wengine wanne wamefungua kesi katika Mahakama ya Haki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACJ) dhidi ya Serikali ya Tanzania, wakidai kuwekwa kizuizini kinyume cha Sheria, kunyimwa kuingia nchini na kufukuzwa kati ya Mei 18 hadi 19, 2025, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
Kundi hilo ambalo pia linajumuisha Wanaharakati na Watetezi wa Haki za Binadamu wanne ambao ni Gloria Kimani, Lynn Ngugi, Hussein Khalid na Hanifa Adan wamedai kuwa haki zao kama raia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zilikiukwa waziwazi walipozuiwa kuingia Tanzania kushuhudia kesi ya uhaini dhidi ya Kiongozi wa Upinzani, Tundu Lissu
Aidha, Kesi hiyo inatarajiwa kuhamishiwa Makao Makuu ya EAC - Arusha ambako tarehe ya kusikilizwa itapangwa na Mahakama hivi karibuni
Soma https://jamii.app/KenyaKuiburuzaTZ

👍
😂
❤️
🙏
❤
💪
🫶
38