
JamiiForums
June 11, 2025 at 03:34 PM
SINGIDA: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kudai baadhi ya Maafisa Utumishi na Ofisi ya Mkurugenzi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wanachelewa kupitisha barua za uhamisho wa Watumishi na kutoa wito kwa UTUMISHI au TAMISEMI kufuatilia na kuchukua hatua, ufafanuzi umetolewa
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama imesema inatekeleza mchakato wa uhamisho wa Watumishi kwa mujibu wa taratibu na Kanuni za Utumishi wa umma kupitia Mfumo rasmi wa maombi ya Uhamisho (Employee Self Service ESS)
Kuhusu Watumishi wanaohama kufuata wenza wao, Halmashauri hiiyo imeeleza mara ya mwisho walipokea barua Mei 2025 na zile zilizokidhi vigezo zimepitishwa na wahusika wamekabidhiwa kwa ajili ya Utekelezaji
Soma https://jamii.app/MkalamaDC

❤️
😂
🙏
💪
😢
😭
🥰
13