
JamiiForums
June 12, 2025 at 07:44 AM
Rais William Ruto amesema Usalama wa Kenya ni Haki ya Wananchi, hivyo Wahalifu wote wawe Raia au Maafisa wa Usalama wa Taifa lazima wawajibishwe Kisheria
Kauli hiyo ni baada ya uchunguzi wa Mwili wa Mwanaharakati na Mwanamitandao Albert Ojwang' aliyedaiwa kufariki kwa kujigonga ukutani, kubaini kuwa aliteswa na kupigwa vibaya akiwa chini ya ulinzi wa Polisi
Aidha, Bunge liliahirisha shughuli zake kujadili suala hilo ambapo Waziri wa Mambo ya Ndani, IGP, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) waliitwa kujibu maswali kuhusu kesi hiyo, ambapo Taasisi ya Kusimamia Utendaji wa Polisi (IPOA) ilieleza Mifumo ya CCTV katika ofisi ya Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi alipokuwa akishikiliwa Albert ilichezewa
Zaidi https://jamii.app/RutoUhalifu
Video Credits: BBC Swahili
❤️
👍
😢
🇹🇿
💀
🙏
😂
😮
29