
JamiiForums
June 12, 2025 at 02:51 PM
Serikali imesema Mwaka 1961 tulikuwa na Shule za Msingi 3,270, Walimu 9,885 na Wanafunzi 486,470. Shule za Sekondari 41, Walimu 764 na Wanafunzi 11,832. Vyuo vya Ualimu 8, Walimu 164, na Wanafunzi 1,723, Chuo kikuu kimoja, Wahadhiri 6 na Wanafunzi 14.
Hadi kufikia Mwaka 2024, Tanzania ilifikisha Shule za Msingi 20,533, Walimu 229,840 na Wanafunzi 11,391,185. Shule za Sekondari 6,269, Walimu 128,686 na Wanafunzi 3,314,198. Vyuo vya Ualimu 65, Walimu 1,633 na Wanafunzi 16,002, Vyuo Vikuu 79, Wahadhiri 8,625 na Wanafunzi 334,854
Serikali pia imeendelea kuongeza Vyumba vya Madarasa ya Elimu ya Msingi kutoka 128,425 Mwaka 2020 hadi Madarasa 155,330 Mwaka 2024 na Vyumba vya Madarasa ya Elimu ya Sekondari kutoka 46,928 Mwaka 2020 hadi 81,052 Mwaka 2024.
Soma https://jamii.app/BajetuKuu2025

😂
👍
❌
❤️
🎉
💪
🖕
😢
😮
🙌
15