IslamicForum
May 24, 2025 at 06:21 AM
Sheikh Waleed Al-Huwairini ameaga dunia mwaka mmoja baada ya kuachiliwa kutoka jela ya Saudia.
Mnamo Septemba 12, 2017, vikosi vya usalama vya Saudi vilivamia nyumba yake na kumzuilia kufuatia kampeni iliyoenea ya ukamataji uliofanywa na mamlaka.
Wakati wa kuwekwa kizuizini. Sheikh Waleed alinyimwa haki ya kutembelewa na familia yake au kuwasiliana nao, na alinyimwa pia haki ya kuteua wakili wa kumtetea. Alifungwa katika kifungo cha upweke katika gereza la al-Ha’ir.
Alihukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani, kifungo ambacho kiliisha rasmi Septemba 2022. Hata hivyo, kuachiliwa kwake kulicheleweshwa kwa karibu mwaka mmoja na nusu, na hatimaye akaachiliwa mnamo Juni 2024. Afya yake ilidhoofika kwa sababu ya kupuuzwa na matibabu na hali ngumu ya kifungo chake.
#saudiarabia