JamiiForums

JamiiForums

716.2K subscribers

Verified Channel
JamiiForums
JamiiForums
June 13, 2025 at 12:10 PM
SONGWE: Mdau anadai changamoto ya foleni ya magari ya mizigo mpaka wa Tanzania na Zambia upande wa Tunduma ni kero kubwa, inakwamisha Uchumi wa Watu wengi na kuwafaidisha wachache Anadai kuna Kiongozi wa Usalama hapo anamiliki eneo la kuegesha (parking) anatoza Sh 10,000 kwa siku badala ya Tsh. 5,000 inayotozwa kwingine na kwamba Mwanausalama huyo anatoa kipaumbele kwa Wateja wake kuvusha magari huku wengine wakibaki kucheleweshewa mchakato Pia, Mdau anadai hali ya Watumishi kukosa uadilifu inachangia foleni kwa kuwa michakato inafanyika kwa kasi ndogo kwa baadhi ya Maafisa kujali maslahi binafsi Ikumbukwe, Aprili 2025, Mkuu wa Mkoa, Daniel Chongolo aliunda Kamati Maalumu kuchunguza msongamano huo ambapo baadhi ya Wadau walimwambia inatengenezwa na Watu wachache kwa sababu wanazozijua wao Soma https://jamii.app/TundumaFoleniJuni Video Credits: CHAWAMATA TV
👍 😂 😮 😢 ❤️ 16

Comments