🧣THE REAL VOICE🧣
🧣THE REAL VOICE🧣
June 15, 2025 at 10:11 AM
HAPPY FATHER'S DAY ❤️ Ndugu zangu najua nyinyi mtaungana na mimi kwenye hili kwamba kuwa baba sio jambo rahisi katika uhalisia wake. Kadri unavyozidi kuwa mwenye akili kama mwanaume, ndivyo unavyoanza kuelewa na kumheshimu baba yako zaidi na kumsamehe kwa kila kitu... Taratibu unaanza kuheshimu sadaka yake na namna alivyojitoa kwenu haijalishi uhusiano au maelewano yake na mama yako Inawezekana kabisa ulipokuwa mdogo, ulimhukumu baba yako. Hukuielewa sababu ya yeye kuwa mbali kihisia…na mama yako Au hata sababu ya kuwa na uchovu kila wakati. Sababu ya kushindwa kuonyesha upendo jinsi ulivyotamani. Uliangalia tu yale yaliyokosekana na sio yale aliyokuwa amebeba moyoni. Sasa umekua mtu mzima Umeshajua maana ya kuwa na majukumu. Umeshahisi uzito wa bili, matarajio, shinikizo, na kimya… Bila shaka unaanza kumuona kwa macho tofauti, kama amekwisha fariki unatamani ungepata angalau dakika tano umwambie "Baba nisamehe kwa kushindwa kukuelewa" unatamani japo ungemkumbatia na kumwambia Mshua hakika ulipambana kadiri ulivyoweza. Huyo mzee aliacha ujana wake ili wewe uendelee kuishi vizuri Alijitolea ndoto zake, amani yake, na huenda hata utambulisho wake… Ili tu kuwe na chakula mezani. Viatu miguuni mwako. Paa juu ya kichwa chako. Huenda hakuwahi kusema “nakupenda.” Huenda hakujua jinsi ya kuonyesha hilo. Lakini alilionyesha kwa vitendo. Katika kazi ndefu zisizo na mwisho. Katika ustahimilivu wa kimya. Katika kubaki, hata pale alipokuwa akivunjika ndani kwa ndani. Wakati mwingine wanaume wanabeba maumivu kwa muda mrefu....🙌🏾 Ndiyo, huenda alikosea. Huenda hakuwa mkamilifu. Lakini alijitahidi kwa kutumia chochote alichokuwa nacho kwa kadiri ya uwezo wake Na wakati mwingine, upendo huonekana kama msamaha. Kadri unavyoendelea kukua… Ndivyo unavyoelewa ugumu wa kuwa mwanaume katika dunia hii. Unatambua mzigo wa kubeba familia. Na unaanza kumheshimu mtu anae itwa baba Hata kama alikuwa na mapungufu. Naomba tuelewane hapa hii siyo kuhusu kusahau maumivu. Ni kuhusu kuona picha kubwa zaidi. Heshimu kimya chake kusamehe mapungufu yake na kuheshimu sadaka yake. Maana ipo siku, huenda ukawa mwanaume ambaye mwanao anajaribu kumwelewa. Na utatarajia achague rehema badala ya hukumu. Baba yako huenda haitaji msamaha wako. Lakini anaweza kuhitaji kumbatio lako. Simu yako. Heshima yako. Fanya hivo tafadhali kama angali hai Nguvu ya kweli ni kusamehe. Akili ya kweli ni huruma. Uanaume wa kweli ni heshima. Mheshimu baba yako. Hata kama hakufanikisha kila kitu. Alikupa maisha kwa vyovyote vile..

Comments