
Side Makini Blog
June 13, 2025 at 11:15 AM
Msanii maarufu Billnass amesema kuwa hajawahi kulipwa hata senti moja kwa wimbo wake "Puuh", licha ya kuwa na zaidi ya streams milioni 36 kwenye YouTube, Spotify, na Audiomack!
🧠 Kupitia Instagram, Billnass alisema “Sijisikii vibaya, lakini hii ni changamoto kubwa kwa wasanii wengi – ujanja wa mikataba na uelewa mdogo wa mifumo ya kidigitali unatuumiza.”
🤔 Kama Billnass mwenye followers na hits anapoteza mapato, je chipukizi hali yao ikoje?
📣 Tunatoa wito kwa mashirika ya wasanii, serikali na wadau kuweka nguvu kwenye:
– Elimu ya biashara ya muziki
– Ushauri wa kisheria
– Uwazi kwenye mapato ya kidigitali
📢 WASANII: LINDENI KAZI ZENU!
#sidemakiniblog
