Bank of Tanzania

Bank of Tanzania

293.7K subscribers

Verified Channel
Bank of Tanzania
Bank of Tanzania
June 18, 2025 at 11:29 AM
Bodi ya Wakurugenzi ya Benki Kuu ya Tanzania, ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye pia ni Gavana wa Benki Kuu, Bw. Emmanuel Tutuba, imefanya ziara katika mradi wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, jijini Dodoma. Ziara hiyo imefanyika tarehe 17 Juni 2025, ambapo Msimamizi wa Mradi, Mhandisi Kedrick Chawe, alieleza kuwa mradi huo unatekelezwa chini ya usimamizi wa TANROADS kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Ujenzi huo unajumuisha njia ya kuruka na kutua ndege (runway), jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege, pamoja na miundombinu mingine muhimu. Kukamilika kwa uwanja huu kunatarajiwa kuchochea ukuaji wa sekta ya utalii, kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, kurahisisha usafirishaji wa mizigo, na hivyo kuongeza mapato ya serikali. Aidha, mradi huu utaimarisha hadhi ya Dodoma kama mji mkuu na kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa taifa. https://www.instagram.com/reel/DLCil3zO4RL/?igsh=MWYzbThydjd4NmRi
👍 ❤️ 🇹🇿 🫱‍🫲 7

Comments