
JamiiForums
June 17, 2025 at 04:15 PM
DAR: Kesi ya Marejeo iliyopo Mahakama Kuu Dar es Salaam iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa, Tundu Lissu dhidi ya Jamhuri ambayo ilipangwa kutajwa leo Juni 17, 2025 imeahirishwa hadi Juni 27, 2025.
Shauri hilo lilipangwa kusikilizwa kwa njia ya Mtandao mbele ya Jaji Mkwizu, lakini Mahakama imeagiza kuwa litakapotajwa tena Juni 27, Lissu anatakiwa kufikishwa Mahakamani
Katika shauri hilo Lissu anaoimba Mahakama kufanya marejeo ya mwenendo wa Kesi ya tuhuma za 'kutoa taarifa za uongo Mtandaoni', ambayo inasikilizwa na Hakimu Mfawidhi Muhini katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Soma https://jamii.app/KesiMarejeoLissu

❤️
😢
👍
🙏
😮
✌
😭
21