NURU YA UPENDO
NURU YA UPENDO
June 16, 2025 at 03:25 PM
*MAOMBI YA USIKU.* JUMATATU[16.06.2025]. JINA LA BWANA WETU YESU KRISTO LIBARIKIWE SANA. KARIBU KATIKA MAOMBI YA USIKU VIPENGELE VITATUMWA KILA SIKU USIKU UNAOMBA WAKATI WA KULALA UKISHAMALIZA KULA CHAKULA CHAKO SIO MAOMBI YA MFUNGO. *NENO KUU* :YESU NI MPATANISHI NA MPONYAJI. Isaya 53:5 "Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, *Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona* ." ✓ *VIPENGELE VYA MAOMBI YA LEO JUMATATU.TUNAOMBA* MAOMBI YA KUOMBEA WAGONJWA👇👇.[ 1.Maombi ya rehema na msamaha Kwa Wagonjwa . ●Omba Rehema na Toba kwa wagonjwa wote walioko Hospitalini na Sehemu Nyingine ata kama wewe ni Mgonjwa omba Rehema na Toba mbele za Mungu kama Unaweza Kuomba . “Ee Bwana, unihurumie, unionyeshe nafsi, uniponye, kwa kuwa nimekutenda dhambi.” – Zaburi 41:4 2. Maombi ya faraja na nguvu kwa Wagonjwa . ●Omba Mungu Wagonjwa wote awape faraja , Nguvu hata wakati wa Mateso Na Damu Yake Ipite katikati Yao. “Bwana humtegemeza mtu aliye kitandani mwa ugonjwa; Katika ugonjwa wake humfanyia tandiko lake.” – Zaburi 41:3 ■Ondoa Vizuizi Vya uponywaji vilivyoshikilia Wagonjwa Kwa Jina la Yesu. ■kemea Roho za Wachawi zinazotuma Magonjwa na Madhahabu za ukoo hamisha kwa Jina La Yesu , Ukuta wa Laana uliowekwa Bomoa kwa Jina la Yesu . ■Kataa Magonjwa sugu, Magonjwa Ya Kurithi kwa Damu Ya Yesu ..Juu Ya Familia Yako, Juu Ya Watoto, n.k. *N.B* : Vipengele vya Maombi vitatumwa Kesho. ✍🏽 *NA IKIWA UNAHITAJI LAKO LA KUSHIRIKISHANA, MAOMBEZI, KUOKOKA, UKIONA AMANI TUMA. *_[Wagalatia 6:2]_* *Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.* *_[Wakolosai 3:15 ]_* **Na amani ya Kristo iamue ndani yenu,ndiyo mliyo itiwa katika mwili mmoja* . 0793006146 . ✓Mungu akubariki.
🙏 ❤️ 👍 👏 23

Comments