TRA TANZANIA
                                
                                    
                                        
                                    
                                
                            
                            
                    
                                
                                
                                June 18, 2025 at 07:26 PM
                               
                            
                        
                            TRA YAENDELEA NA KAMPENI YA ELIMU YA KODI NA KUSIKILIZA CHANGAMOTO  
Naibu Kamishna wa Walipakodi Wakubwa Bw. Gabriel Kimweri  amesema amefarijika sana na ujio wa Watendaji wa Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya mkoani Geita (GGM) katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa lengo la kuwasilisha changamoto zao na kujadiliana mambo mbalimbali ya kodi. 
Ameyasema hayo leo tarehe 18.06.2015 katika Kikao ambacho ni sehemu ya muendelezo wa Kampeni ya Elimu kwa  Mlipakodi na kusikiliza changamoto yenye lengo kuwahudumia walipakodi kwa karibu zaidi na kutatua changamoto zao.  
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa kodi wa Kampuni ya Uchimbaji wa madini ya Ashanti ambayo ni Kampuni mama ya GGM na kiongozi wa ujumbe huo Bw. Gelishan Naicko amesema anaishukuru TRA kupitia Idara ya Walipakodi Wakubwa kwa ushirikiano wao wanaoendelea kuonesha  jambo linalowasaidia wao kuendelea kulipa kodi zaidi na kwa wakati bila ya mgogoro wowote.
                        
                    
                    
                    
                        
                        
                                    
                                        
                                            👍
                                        
                                    
                                    
                                        3