
Dr. BUDODI
June 13, 2025 at 09:01 PM
Mlango wa kizazi(Cervix) hulindwa na ute ambao husaidia mbegi za kiume kusafiri kiurahisi kipindi cha ovulation kuelekea kwenye mji wa mimba. Ikitokea ute huu hauna sifa zinazosaidia mbegu kisafiri na pengine hata kuzidhuru mbegu basi inakua vigumu kwa mwanamke kubeba mimba. Ute usiofaa kwenye mlango wakizazi, unaathiri 5-10% ya wanawake wanaoshindwa kupata ujauzito, huku kujifunga kwa mlango wa uzazi(Cervical Stenosis) ikichangia kwa ~3-5%. Magonjwa haya hufanya iwe vigumu kwa mwanamke kuzaa..Bila matumizi ya njia za kisasa za upandikizaji ni vigumu kwa wanawake hawa kupata mimba kwa njia za kawaida.
