Dr. BUDODI WhatsApp Channel

Dr. BUDODI

91 subscribers

About Dr. BUDODI

Afya karibu yako. Dondoo za Afya Elimu na Vifaa tiba. afya bora ndio msingi wa furaha Maishani

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/4/2025, 2:04:38 PM

Fikiria ovari zako kama ghala hivo kuna kiwango fulani cha mayai kisichoweza kuongezeka, lakini ghafla mayai hayo inapungua na kuisha kabla ya muda uliotakiwa. Hali hii hutambulika kitaalamu kama Premature Ovarian Insufficient (POI), hali ambayo huathiri wanawake ni changamoto kubwa kwa wale wanaotamani kuitwa mama. Ni kama mwili wako unaacha kupevusha mayai kabla hujafikisha miaka 40, matibabu ya kisasa kama upandikizaji huongeza tumaini kwa wanawake wenye hili tatizo. Hebu tuchunguze POI ni nini, kwa nini inazuia ujauzito, na jinsi unavyoweza kuvuka kikwazo hiki na kupata mtoto wako.

Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/3/2025, 1:53:09 PM

https://youtube.com/shorts/dJjmp5mCVLY?si=UF2ZypSfszdKz4IG

Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/4/2025, 2:16:51 PM
Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/4/2025, 2:16:36 PM

*POI inatokeaje?* POI inatokea wakati ovari zinashindwa kufanya kazi vizuri kabla ya umri wa miaka 40, zikipunguza idadi ya mayai na kutoa homoni za estrojeni kidogo. Ovari ni viungo vinavyohifadhi na kutoa mayai, na pia hutoa homoni zinazodhibiti hedhi na ujauzito. Katika POI, ovari hupoteza uwezo wake wa kutoa mayai au homoni za kutosha, na kusababisha hedhi kuvurugika au kukosekana kabisa. POI inaweza sababishwa na magonjwa ya kurithi(kama Turner syndrome), magonjwa ya kingamwili ambapo mwili unashambulia ovari, au madhara yatokanayo na matibabu ya saratani kama chemotherapy au radiotherapy. Dalili zinaweza kujumuisha kuhisi fukuto(joto la ghafla mwilini (hot flashes), uchovu, au hedhi zisizo za kawaida, ambazo mara nyingi hugunduliwa katika miaka ya 20 au 30. Viwango vya juu vya homoni ya FSH (>20 IU/L) na AMH ya chini (<0.5 ng/mL) huashiria kufeli kwa ovari. *POI inasababishaje utasa?* POI inapunguza sana idadi ya mayai yaliyopo kwa mwanamke(kila mwanamke huzaliwa na kiwango fulani cha mayai ambacho huwa hakiongezeki), na mara nyingi upevushaji haufanyiki, hii inafanya iwe vigumu kwa mbegu za kiume kuungana na yai. Hata kama upevushaji ukitokea, mayai yanayopevushwa mara nyingi hayana ubora wa kutosha, na hivyo huongeza hatari ya kuharibika kwa mimba kwa ~30-50%. Hali hii inafanya iwe vigumu kwa mwanamke kubeba mimba bila msaada wa matibabu. *Ipi ni njia nzuri na salama ya kumsaidia mgonjwa wa POI?* Njia za upandikizaji kama IVF na IUI hutoa matokeo mazuri kwa wanawake wenye changamoto hii. Kwa wanawake ambao upevushaji umekoma kabisa na imeshindikana kuchochea kwa homoni, basi hawa wanaweza kuzaa kwa kuchangiwa mayai (Donor Egg IVF). IVF ya Kawaida inajaribu kuchukua mayai yaliyobaki ikiwa ovari bado zina uwezo mdogo, lakini hii ni nadra kwa POI. *Mambo Yanayoathiri Ufanisi wa njia za upandikizaji.* * _Umri_ : IVF ya kuchangiwa mayai(Donor Egg IVF) ina ufanisi wa ~50-60% kwa kila mzunguko, bila kutegemea umri wa mpokeaji. IVF ya mayai ya mama husika ina ufanisi wa chini ya 5% kwa POI kutokana na mayai machache na yasiyo bora. * _Afya ya mji wa mimba:_ Unene wa endometrium(kuta za mji wa mimba) chini ya 7 mm hupunguza uwezekano wa kupandikizwa kwa ~20-30%. * _Umri wa Mchangiaji:_ Mayai kutoka kwa mchangiaji mwenye umri chini ya miaka 35 yana ufanisi wa ~50-60%, lakini wachangiaji wakubwa hupunguza ufanisi hadi ~30-40%. * _Viwango vya Homoni:_ FSH ya juu (>20 IU/L) huonyesha ufanisi wa karibu sifuri kwa IVF ikiwa mayai ya mama husika yatatumika. * _Matibabu ya Awali:_ Chemotherapy inaweza kuharibu mji wa mimba, ikipunguza ufanisi wa IVF kwa ~10-20%. *Ushauri wa kitaalam* Ikiwa una dalili za POI kama hot flashes au hedhi zisizo za kawaida kabla ya miaka 40, wasiliana na daktari haraka kwa vipimo vya damu (FSH, AMH) na uchunguzi zaidi. POI mara nyingi inahitaji IVF. Ni vema kuanza mapema, kwani afya ya mji wa mimba hupungua kadili umri unavyoongezeka. Matibabu ya homoni (kama estrojeni) yanaweza kutayarisha mji wa mimba kwa upanikizaji. Chagua kliniki ya uzazi yenye uzoefu kwa matokeo mazuri. Ushauri wa kisaikolojia ni muhimu, kwani POI huathiri sana saikolojia. Kwa maribabu sahihi, unaweza kuitwa mama hata ikiwa una changamoto ya POI.

Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/3/2025, 1:52:07 PM
Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/4/2025, 2:16:51 PM
Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/4/2025, 2:16:53 PM
Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/4/2025, 2:16:52 PM
Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/3/2025, 1:52:15 PM
Post image
Image
Dr. BUDODI
Dr. BUDODI
6/3/2025, 1:52:04 PM
Post image
Image
Link copied to clipboard!