Duro Crypto
Duro Crypto
June 21, 2025 at 04:03 AM
*Hatari Zake ni Zipi?* 1. *Kupoteza haraka* : Bei inabadilika ghafla sana, ukiingia vibaya unapoteza. 2. *Inahitaji kuwa macho muda wote:* Huwezi kwenda kumsalimia jirani wakatu huku uko kwenye trade.😀 3. *Inachosha kichwa:* Huwa inahitaji maamuzi ya haraka haraka, presha pia ni kubwa. 4. *Ada nyingi:* Kila unavyofanya trade kuna ada ya platform, ikizidi huwezi kuona faida. 5. *Mashindano na bots: Kuna mashine* zinazofanya hizi trades kwa sekunde, ni ngumu kushindana nazo kwa mikono. *Timeframe* Scalpers hutumia timeframe ndogo kama dakika 1, dakika 5 au dakika 15. Wengine hata hutumia sekunde 15, lakini hapa wanakutana na bots. Mara nyingi, scalper huanza kwa kuangalia timeframe kubwa (kama saa 1 au siku 1) ili kujua mwelekeo wa soko, kisha huingia timeframe ndogo kutafuta fursa. *Technical Analysis kwa Scalping* Scalping inategemea sana technical indicators. Scalpers huangalia: Candlestick patterns Moving Averages RSI Bollinger Bands VWAP Fibonacci retracement MACD Wengine hutumia order book, volume profile, open interest, na wengine hutengeneza indicators zao wenyewe.

Comments