𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
June 16, 2025 at 05:36 AM
Kitunguu swaumu kina umuhimu mkubwa katika afya ya binadamu kutokana na uwezo wake wa kutoa kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali. Kina virutubisho vingi kama vile vitamini C, B6, madini ya selenium na manganese. Pia kina kemikali za asili ambazo huongeza kinga ya mwili, kusaidia kushusha shinikizo la damu na kupunguza Mafuta Mwilini. 🦠Kitunguu swaumu husaidia pia katika kupambana na bakteria na fangasi, hivyo ni msaada katika tiba ya maambukizi madogo. 🚩Husaidia kusafisha damu, kuboresha mzunguko wa damu, na huweza kuchangia kuboresha afya ya moyo. 💪Wengine hutumia kwa ajili ya nguvu za mwili na kuongeza hamu ya kula. Pia, matumizi ya mara kwa mara ya kitunguu swaumu huweza kusaidia kupunguza hatari ya kupata magonjwa ya saratani kwa baadhi ya watu. ---------------------------------------------------- Dkt Fedrick, Telehealth Clinician #afyayauzazi#femclinic_hc#tunajalinakuthaminiafyayako#upati#drfedrickntashobo#clinician#sexualhealth&reproductivehealthcoach#vochadaychallenge
Image from 𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔: Kitunguu swaumu kina umuhimu mkubwa katika afya ya binadamu kutokana n...
👍 ❤️ 3

Comments