𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔 WhatsApp Channel

𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔

681 subscribers

About 𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔

𝖯𝖺𝗍𝖺 𝖧𝗎𝖽𝗎𝗆𝖺 𝗒𝖺 𝖣𝖺𝗄𝗍𝖺𝗋𝗂 𝖪𝗂𝗀𝖺𝗇𝗃𝖺𝗇𝗂 ,𝖧𝗎𝖽𝗎𝗆𝖺 𝗓𝖺 𝖺𝖿𝗒𝖺 𝖭𝗒𝗎𝗆𝖻𝖺𝗇𝗂 - 𝖧𝗈𝗆𝖾 𝖼𝖺𝗋𝖾 𝗌𝖾𝗋𝗏𝗂𝖼𝖾 ,𝖣𝗈𝗄𝖾𝗓𝗈 𝗓𝖺 𝖠𝖿𝗒𝖺 𝗒𝖺 𝗎𝗓𝖺𝗓𝗂 𝗇𝖺 𝖠𝖿𝗒𝖺 𝗄𝗐𝖺 𝖴𝗃𝗎𝗆𝗅𝖺 𝗇𝖺 𝖬𝖺𝗍𝖺𝗇𝗀𝖺𝗓𝗈 𝖬𝗎𝗁𝗂𝗆𝗎 𝗄𝗎𝗁𝗎𝗌𝗎 𝖧𝗎𝖽𝗎𝗆𝖺 𝖹𝖾𝗍𝗎 𝗄𝗐𝖺 𝖩𝖺𝗆𝗂𝗂. 𝖯𝖺𝗆𝗈𝗃𝖺 𝗍𝗎𝖻𝗈𝗋𝖾𝗌𝗁𝖾 𝖠𝖿𝗒𝖺 𝖹𝖾𝗍𝗎 𝗄𝗐𝖺 𝗄𝗎𝗉𝖺𝗍𝖺 𝖳𝖺𝖺𝗋𝗂𝖿𝖺 𝖬𝗎𝗁𝗂𝗆𝗎 𝗇𝖺 𝖲𝖺𝗁𝗂𝗁𝗂. 𝖱𝖺𝗍𝗂𝖻𝖺, 𝗄𝗂𝗅𝖺 𝖲𝗂𝗄𝗎 𝖩𝗎𝗆𝖺𝗍𝖺𝗍𝗎 𝖬𝗉𝖺𝗄𝖺 𝖩𝗎𝗆𝖺𝗆𝗈𝗌𝗂. 𝖹𝗂𝗇𝗀𝖺𝗍𝗂𝖺 𝖬𝖽𝖺 𝗇𝗂 𝗄𝗎𝖺𝗇𝗓𝗂𝖺 𝖲𝖺𝖺 𝖬𝖻𝗂𝗅𝗂 𝖠𝗌𝗎𝖻𝗎𝗁𝗂 𝖬𝗉𝖺𝗄𝖺 𝖲𝖺𝖺 𝖪𝗎𝗆𝗂 𝖩𝗂𝗈𝗇𝗂. 𝖳𝖾𝗆𝖻𝖾𝗅𝖾𝖺 𝖳𝗈𝗏𝗎𝗍𝗂 𝖸𝖾𝗍𝗎 𝖭𝖽𝗈𝗀𝗈 https://linktr.ee/femclinic_hc 𝖤𝗇𝖽𝖾𝗅𝖾𝖺 𝗄𝗎𝗐𝖺𝗌𝗂𝗅𝗂𝖺𝗇𝖺 𝗇𝖺𝗌𝗂 𝗄𝗐𝖺 𝖧𝗎𝖽𝗎𝗆𝖺 𝖡𝗈𝗋𝖺 𝗓𝖺 𝖠𝖿𝗒𝖺!❤

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 4:40:24 PM

https://www.instagram.com/p/DKr9XbMtJUk/?igsh=NHhwZm56ZHQxbjRq

𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 4:29:42 PM

Habarini za Usiku ,Siku ya Kesho Dkt Fedrick Anapatikana  kwaajili ya Huduma ya Online  Consultation .Kuanzia sasa unaweza kuweka Miadi na Daktari 🗓10 June 2025 🤑Huduma Hii ni Bure! 😷Matibabu ya Ugonjwa wa Typhoid 🌐Weka Miadi https://t.co/xYNd016N2H ⏰Kuanzia Saa 4 Asbh Mpaka Saa 6 Mchana Dkt Fedrick, Telehealth Co Kwa kesi zote zinazosubiri ufuatiliaji tafadhali usisite kupiga Simu. 0747 290 565 , 0688 971 032 au Chati na Huduma kwa wateja WhatsApp https://wa.me/255747290559 #afyayauzazi#femclinic_hc#tunajalinakuthaminiafyayako#upati#drfedrickntashobo#clinician#sexualhealth&reproductivehealthcoach#vochadaychallenge

Post image
Image
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/10/2025, 3:27:51 AM

*Wapendwa, Habarini za Asubuhi! "Usiku ni Nusu ya kifo kuamka Salama ni Neema" Je, umeanza Siku yako kwa Sala ya kumshukuru Muumba?*

❤️ 👍 2
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 5:50:11 PM

Kuvalisha uume kondomu ni hatua muhimu katika kujikinga na magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa. Kondomu inapaswa kuvalishwa kabla ya uume kuingia kwenye uke, mdomo au sehemu nyingine yoyote ya kufanyia ngono. Hakikisha umechagua kondomu mpya, ambayo haijaisha muda wake wa matumizi na haijachanika. Fungua paketi kwa uangalifu bila kutumia meno au vitu vyenye ncha kali. Shika kondomu kwa upande wa ncha iliyo na kimoja kilichojaa hewa (teat) na bonyeza sehemu hiyo kwa vidole ili kutoa hewa na kuzuia kondomu kupasuka. Weka kondomu juu ya kichwa cha uume uliosimama, kisha ikunjue taratibu mpaka chini ya uume huku ukiendelea kushikilia ncha ya juu. Baada ya kumaliza tendo, ondoa kondomu kabla uume haujalegea kabisa, kwa kuishika kwenye shina la uume ili isije ikateleza. Funga kondomu na kuitupa kwenye pipa la taka, usiitumie tena. Kutumia kondomu kwa usahihi husaidia sana katika afya ya uzazi na kujikinga dhidi ya maambukizi. -------------------------------------- Article by: Dkt Fedrick, Telehealth Co

👍 1
Video
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 5:08:56 AM

Mazoezi ya asubuhi huamsha mwili na kuupa nguvu ya kuanza siku vizuri. Husaidia kuimarisha mzunguko wa damu, kuongeza kiwango cha oksijeni mwilini, na kuchochea uzalishaji wa homoni zinazopunguza msongo wa mawazo kama endorphins. Mazoezi pia huongeza kasi ya kuchoma mafuta, kusaidia udhibiti wa uzito, na kuboresha usingizi wa usiku. Kwa kufanya mazoezi asubuhi, mwili huwa makini zaidi, kiwango cha nishati huongezeka, na mtu hujihisi vizuri kimwili na kiakili siku nzima. -------------------------------------- Dkt Fedrick, Telehealth Co #afyayauzazi#femclinic_hc#tunajalinakuthaminiafyayako#upati#drfedrickntashobo#clinician#sexualhealth&reproductivehealthcoach#vochadaychallenge

Post image
Image
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 5:51:56 PM

Kama hauwezi kudhibiti tamaa za Ngono Hautaweza kudhibiti Mambo Mengi kwenye maisha yako. Kichwa na Mdomo wa chini havijawahi kumuacha mtu salama. Take care, Good Night. See you Tomorrow 👁️ -------------------------------------- Article by: Dkt Fedrick, Telehealth Co

❤️ 3
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/10/2025, 5:21:29 AM

Je, umewahi kukumbwa na tatizo la meno kuoza (Dental Caries)?

👍 1
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/10/2025, 5:19:01 AM

Dental caries hudhibitiwa kwa kuhakikisha usafi mzuri wa kinywa kila siku kwa kupiga mswaki angalau mara mbili kwa siku na kutumia dawa ya meno yenye fluoride. Ni muhimu pia kupunguza ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi. Kutembelea daktari wa meno mara kwa mara kwa ukaguzi na kusafisha meno kitaalamu husaidia kugundua matatizo mapema. Matumizi ya vyakula vyenye madini ya kalsiamu na vitamini D pia kunasaidia kudumisha afya ya meno. -------------------------------------- Dkt Fedrick, Telehealth Co #afyayauzazi#femclinic_hc#tunajalinakuthaminiafyayako#upati#drfedrickntashobo#clinician#sexualhealth&reproductivehealthcoach#vochadaychallenge

Post image
👍 1
Image
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 3:55:04 PM

Typhoid Fever ni ugonjwa wa maambukizi unaosababishwa na bakteria anayeitwa *Salmonella Typhi*. Bakteria huyu huingia mwilini kwa njia ya chakula au maji machafu yaliyo na kinyesi cha mtu aliyeambukizwa. Ugonjwa huu huathiri zaidi mfumo wa chakula, lakini pia unaweza kusambaa kwenye damu na sehemu nyingine za mwili. Dalili za homa ya tumbo huanza taratibu na ni pamoja na homa ya juu inayoongezeka polepole, maumivu ya kichwa, uchovu, kukosa hamu ya kula, kichefuchefu, kuharisha au kuvimbiwa, maumivu ya tumbo, na wakati mwingine vipele vidogo nyekundu kifuani. Bila matibabu, hali inaweza kuwa mbaya zaidi na kusababisha madhara kama kutoboka kwa utumbo au maambukizi ya damu(Sepsis) Ni muhimu kunywa maji ya kutosha ili kuepuka upungufu wa maji mwilini. Ili kujikinga, ni muhimu kunywa maji safi na salama, kula chakula kilichoandaliwa vizuri, kuosha mikono mara kwa mara, na kuhakikisha mazingira ni safi. -------------------------------------- Article by: Dkt Fedrick, Telehealth Co

Post image
Image
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
6/9/2025, 4:57:10 AM

Je, wewe hufanya mazoezi asubuhi?

Link copied to clipboard!