
𝗙𝗘𝗠𝗖𝗟𝗜𝗡𝗜𝗖 𝗛𝗘𝗔𝗟𝗧𝗛𝗖𝗔𝗥𝗘 𝗦𝗘𝗥𝗩𝗜𝗖𝗘, 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔
June 16, 2025 at 01:08 PM
Tikiti maji ni tunda lenye maji Mengi na virutubisho ambavyo vina faida kubwa kwa mwili wa binadamu. Lina kiasi kikubwa cha madini ya potasiamu, vitamini C, vitamini A, na antioxidants kama lycopene.
Ulaji wa tikiti maji husaidia kuimarisha afya ya moyo, kupunguza shinikizo la damu, kuzuia upungufu wa maji mwilini na kusaidia usafirishaji mzuri wa damu.
Lycopene pia husaidia kupunguza hatari ya saratani, hasa ya kibofu cha mkojo na tezi dume. Tikiti linasaidia pia kuboresha afya ya ngozi, macho na mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.
Kwa wanaume, husaidia kuongeza mzunguko wa damu kwenye maeneo ya uzazi na kuongeza nguvu za kiume kwa Namna ya asili.
----------------------------------------------------
Dkt Fedrick, Telehealth Clinician
#afyayauzazi#femclinic_hc#tunajalinakuthaminiafyayako#upati#drfedrickntashobo#clinician#sexualhealth&reproductivehealthcoach#vochadaychallenge
