
TheChanzo
June 19, 2025 at 08:31 AM
*Ni Fursa kwa Klabu Kuunda Upya Bodi ya Ligi*
*Na Angetile Osiah*
Baada ya mgogoro uliodumu kwa zaidi ya mwezi mmoja kati ya klabu ya Yanga, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) na Shirikisho la Soka (TFF), hatimaye Rais wa Jamhuri ya Muungano, Samia Suluhu Hassan, ameamua kutumia busara kuumaliza.
Yanga ilikuwa inapinga kitendo cha Bodi ya Ligi kuahirisha mechi ya Machi 8, 2025, kati yake na Simba bila ya kufuata kanuni, huku chombo hicho kinachosimamia Ligi Kuu kikishindwa kauli ya kutetea uhalali wa uamuzi huo na kupanga tarehe mpya.
Mgogoro huo ulifika hatua ya Yanga kugomea mechi zote za Ligi na kupanua wigo wa madai yake kwa kutishia pia kugomea fainali ya Kombe la CRDB kwa hoja kwamba haijalipwa fedha za zawadi kwa kipindi cha miaka mitatu.
Soma zaidi
https://thechanzo.com/2025/06/19/ni-fursa-kwa-klabu-kuunda-upya-bodi-ya-ligi/
