
Swautu Jamil Islamic Daawa
14 subscribers
About Swautu Jamil Islamic Daawa
Swautu Jamil Islamic Dawa is a Tanzania-islamic record label founded by Daiya Ismail almunadhaf. SJID commercial roster includes Ismail almunadhaf. The label is headquartered at Unguja,fuoni. Zanzibar. Founder : Ismail almunadhaf Founded : 2021. Location : Unguja fuoni, Zanzibar Slogan : We love Qur an, Sunnah, Mawaidha, Nasheed and Islamic spoken word poetry Follow us Instagram : https://www.instagram.com/swautujamilislamicdaawa?igsh=OHZ4MG9hOGFya2Ro facebook : https://www.facebook.com/profile.php?id=61575055906835 Tiktok : tiktok.com/@swautujamil_islamic_dawa Youtube : https://youtube.com/@swautujamilislamicdawa?si=d6hzRBO763dIwf30 ▫️▫️▫️▫️▫️▫️▫️▫️▫️▫️ WELCOME SJID
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Imam Ahmad bin Hanbal (Rahimahullah): alisema "Kama mtu ataazimia kutafuta elimu kwa ajili ya dunia, haitamfaa; lakini akitafuta kwa ajili ya Akhera, basi dunia itakuja kwake kwa hiari." Dr. almunadhaf

NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA. 1.Theluthi ya mwisho ya usiku. Huu ni usiku wa manane usiku mkubwa. Muda huu mweye kuomba dua katu haiwezi kurudi kama anavyosimulia Abuuhurairah رضىالله عنه kuwa Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema " يَنْزِلُ رَبُّنَا كُلَّ لَيْلَةٍ إِلَى السَّمَاءِ الدُّنْيَا حِينَ يَبْقَى ثُلُثُ اللَّيْلِ الآخِرُ فَيَقُولُ مَنْ يَدْعُونِي فَأَسْتَجِيبَ لَهُ وَمَنْ يَسْأَلُنِي فَأُعْطِيَهُ وَمَنْ يَسْتَغْفِرُنِي فَأَغْفِرَ لَهُ " “anashuka Mola wetu aliye tukuka kuja mbingu ya dunia kila usiku pindi inapobaki theluthi ya usiku ya mwisho kisha husema ‘nani ataniomba nimjibu maombi yake, nani antaniomba nimpe na nani ataniomba msamaha nimsamehe”. (amepokea Bukahari, muslim na wengine). 2.Baada ya swala za faradhi. Anayetaka kuomba dua basi aombe baada ya kuswali swala ya faradhi, dua yake itajibiwa. عَنْ أَبِي أُمَامَةَ، قَالَ قِيلَ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَىُّ الدُّعَاءِ أَسْمَعُ قَالَ " جَوْفُ اللَّيْلِ الآخِرُ وَدُبُرَ الصَّلَوَاتِ الْمَكْتُوبَاتِ " Amesimulia Abuu Umama رضىالله عنه kuwa aliulizwa Mtume صلّي الله عليه وسلّم ‘dua gani husikulizwa (zaidi na Allah? Akasema:) usiku mkubwa (theluthi ya mwisho ya usiku) na baada ya swala za faradhi’”. (amepokea tirmith kwa isnad sahihi). 3.Kati ya adhana na iqama. Huu ni muda unaopatikana baada ya kuadhiniwa na mpaka kukimiwa kwa swala. Hapa mwenye kuomba dua itakuwa ni yenye kujibiwa. Amesimulia Anas رضىالله عنه kuwa Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema “hairudishi (haiachi kujibiwa dua) kati ya adhana na iqama”. (amepokea Abuu Daud, Nisai na tirmith kwa isnad sahihi). 4.Wakati wa kusujudi. Hii ni dua inayoomwa wakati mtu akiwa amesujudi, dua hii pia ni yenye kujibiwa. Amesimulia Abuuhurairah رضىالله عنه kuwa Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema “muda ambao mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake ni pale akiwa amesujudi. Basi zidisheni dua (muda huu) na uweni na uhakika kuwa mtajibiwa. (amepokea Muslim na Daud). 5.Muda wa kukutana majeshi kwenye jihad, muda wa kunyesha kwa mvua, muda wa kukimiwa kwa swala na na muda wa kuiona alkaba. Amepokea Abuu Umamah رضىالله عنه kuwa Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema: “hufunguliwa milango ya mbinguni na hujibiwa dua katika maeneo manne (nyakati): muda wa kukutana safu katika jihadi, muda wa kunyesha kwa mvua, muda wa kukimiwa kwa swala na muda wa kuiona alkaba”. (amepokea Tabrany). 6.Siku ya ijumaa. Siku ya ijumaa kuna muda ambao dua hujibiwa bila ya tatizo. Muda huu ni mchache sana na hakuna anaoujua. Zipo riwaya nyingi sana zinataja muda huu. Ila kuna riwaya zinaonesha muda huu ni baada ya swala ya al-’asr mpaka magharib. Ila ukweli ni kuwa muda huu ni mchache sana na haujulikani, jambo la msingi ni kujitahidi kumuomba Allah siku ya ijumaa yote huenda muda huo ungeupata. JIUNGE NA PAGE YETU YA WHATSAPP KUJIFUNZA MENGI KUHUSU UISLAM

https://youtu.be/QE6Grsr-P6s?si=9Taq6je4LIEQO9Kr

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA. 1.kuchunga adabu za dua kama zilivyotajwa hapo juu. 2.Kuwa twahara nje na ndani. Yaani kujiepusha na mambo maovu na machafu ya siri na yasiyo ya siri. Amesema Mtume صلّي الله عليه وسلّم “hakika Allah ni mzuri na anapenda (vitu) vizuri.…”. (amepekea Bukhari na Muslim) Hivyo mtu anatakiwa ahakikishe ni mzuri ndani na nje. 3.kujiweka mbali na yaliyo haramu yote, na kujiepusha kula na kunywa bya haramu au kuvaa vilivyo haramu. Amesema Mtume صلّي الله عليه وسلّم “ukitaka dua maombi yako basi kifanye kizuri chakula chako (kisiwe cha haramu) “ (amepekea Bukhari na Muslim). Na pia katika hadithi ndefu iliyo sahihi katika kuwa mtume anashangaa mtu ambaye chakula chake haramu, kinywaji chake haramu, a mavazi yake haramu. Isitoshe mtu huyu amechafuka na manywele yapo timtim. Vipi atajibiwa dua yake mtu huyu. (amepekea Bukhari na Muslim). 4.Kuzingatia nyakati ambazo dua hujibiwa. Tutaziona hapo mbele. 5.Sifa ya dua yenyewe. Tutaona dua zenye sifa ya kujibiwa. 6.Hali inayozunguruka dua. Tutaona hali ambazo dua hujibiwa. FOLLOW SJID WHATSAPP PAGE KUJIFUNZA MENGI KUHUSU UISLAM

*🕌 HUKMU YA SWALA YA IJUMAA 🕌* Swala ya Ijumaa ni miongoni mwa swala muhimu za faradhi. Na ni wajib kwa kila Muislamu mwanamume ,mwenye akili timamu, alie baleghe ambae hana nyudhuru za kisheria za kumzuia kuetekeleza ibada hiyo. Na sharia imetia mkazo zaidi na kusisitiza kutekelezwa swala ya ijumaa kwa jamaa. Na malipo yake ni makubwa zaidi. *➡️. FADHLA ZA SIKU YA IJUMAA* ↘️. Kupata Thawabu na Malipo kwa kila hatua ya kwenda Msikitini sawa na Mtu aliyesimama kuswali na kufunga Mwaka mzima. Amesema Mtume ﷺ: مَنْ اغْتَسَلَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ وَغَسَّلَ وَبَكَّرَ وَابْتَكَرَ وَدَنَا وَاسْتَمَعَ وَأَنْصَتَ كَانَ لَهُ بِكُلِّ خُطْوَةٍ يَخْطُوهَا أَجْرُ سَنَةٍ صِيَامُهَا وَقِيَامُهَا] رواه الترمذي وأحمد] [Mwenye kuoga na kujisafisha, kisha akaenda Msikitini na mapema na akamkurubia Khatibu na akasikiliza kwa utulivu. Mwenyezi Mungu ﷻ atamlipa kwa kila hatua malipo sawa na Mtu aliyesimama kuswali na kufunga Mwaka mzima] [Imepokewa na Al-Ttirmidhiy na Ahmed].📕 ↘️. Kusamehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu za ziada. Amesema Mtume ﷺ: مَنْ تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الْوُضُوءَ ثُمَّ أَتَى الْجُمُعَةَ فَاسْتَمَعَ وَأَنْصَتَ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجُمُعَةِ وَزِيَادَةُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ] رواه مسلم] [Mwenye kutawadha vizuri, kisha akaja Msikitini na akamsikiliza Khatibu na kunyamaza. Anasemehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu]. [Imepokewa na Muslim.] 📕 ↘️. Kukubaliwa dua katika siku hii tukufu. Amesema ﷺ: فِي الْجُمُعَةِ سَاعَةٌ لَا يُوَافِقُهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ قَائِمٌ يُصَلِّي فَسَأَلَ اللَّهَ خَيْرًا إِلَّا أَعْطَاهُ] رواه مسلم] [ Hakika katika Siku ya Ijumaa kuna wakati, haafikiwi Muislamu na wakati huo hali akiwa anamuomba Allah Kheri, ila Mwenyezi Mungi humpatia]. [Imepokewa na Muslim] 📕 *➡️. ADABU NA SUNNA ZA SIKU YA IJUMAA* 1️⃣.Kuoga na kujisafisha na kupaka manukato mazuri pamoja na kuondosha harufu mbaya mwilini.. Amesema Mtume ﷺ: مَنْ اغْتَسَلَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ غُسْلَ الْجَنَابَةِ ثُمَّ رَاحَ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَدَنَةً] رواه البخاري ومسلم] [ Mwenye kuoga siku ya Ijumaa, Josho la Janaba kisha akaenda Msikitini (na mapema.) Mfano wake ni kama mtu aliyetowa sadaka ya Ngamia] [Imepokewa na Bukhari na Muslim]📗 2️⃣. Kwenda Msikitini mapema na kumkurubia khatibu. Amesema Mtume ﷺ: احْضُرُوا الذِّكْرَ ، وَادْنُوا مِنَ الْإِمَامِ ] رواه أبوداود] [Nedeni mkasali sala ya Ijumaa, na mkae karibu na khatibu]. [Imepokewa na Abuu Daud]📗 3️⃣. Kujishughulisha kwa Kumtaja Allah, kusoma Qur’an, kuomba msamaha, kuomba dua kwa wingi na kumsalia Mtume Muhammad ﷺ. 4️⃣. Kumsilikiza Khatibu kwa utulivu, bila ya kujishughulisha na mambo mengine. Asema Mtume ﷺ: مَنْ تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الْوُضُوءَ ثُمَّ أَتَى الْجُمُعَةَ فَاسْتَمَعَ وَأَنْصَتَ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجُمُعَةِ وَزِيَادَةُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ] رواه مسلم] [Mwenye kutawadha vizuri, kisha akaja Msikitini na akamsikiliza Khatibu na kunyamaza. Anasemehewa Madhambi yake ya wiki mzima pamoja na siku tatu]. [Imepokewa na Muslim.] 📕 *➡️. MAMBO YALIO KATAZWA KATIKA SWALA YA IJUMAA* 1️⃣. Kuja Msikitini kuchelewa na kukata safu kwa kuruka watu, kwa lengo la kutaka kukaa safu ya mbele. Siku moja Mtume ﷺ alimuona mtu akikata safu na kuruka watu; Akamuambia: اجلس فقد آذيت وآنيت] رواه إبن ماجة] [Kaa chini kwa hakika umewaudhi watu na umechelewa.] [Imepokewa na Ibnu Maajah] 2️⃣. Kuwashawishi waja wa Mwenyezi Mungu, kwa kusoma Qur’an kwa sauti kubwa, au kufanya Dhikri kwa sauti ya juu. Mtume ﷺ aliwakataza Masahaba kusoma kwa sauti ya juu, na akawambia; Asisome mmoja wenu Qura’n kwa sauti ya juu kuliko mwingine. 3️⃣. Kuzungumza wakati wa Khatibu anatoa khutbah ya Ijumaa. Amesema Mtume ﷺ: من قال لصاحبه يوم الجمعة والإمام يخطب أنصت فقد لغا] رواه النسائي] [Ukimuambia mwenzako nyamaza na Khatibu akiwa anazungumza, amefanya upuzi]. [Imepokewa na Al-Nnasaai] 📕 *➡️. KHATARI YA KUACHA SWALA YA UJUMAA* Mtume Muhammad ﷺ Amesisitiza na kutilia mkazo juu la suala la kutekeleza swala ya Ijumaa. Na akawatahadharisha Waislamu wanaoacha kutekeleza swala hii. Adhabu kubwa watakayo pata watu hao hapa duniani ni nyoyo zao kuwa ngumu na kupigwa muhuri wa kughafilika. Amesema Mtume ﷺ: لينتهين أقوام عن ودعهم الجمعات، أو ليختمن الله على قلوبهم، ثم ليكونن من الغافلين] رواه مسلم وأحمد والنسائي] [Hawataendelea watu kuacha swala ya Ijumaa, mpaka Mwenyezi Mungu apige muhuri nyoyo zao, kisha watakuwa niwenye kuishi katika mughafala]. [Imepokewa na Muslim na Ahmad na Al-Nnasaai]📘 Ndugu Muislamu, tujihadhari sana na kuacha swala ya Ijumaa, kwasababu adhabu yake ni nzito sana. Moyo ukiwa mgumu, basi mwanadamu anakuwa sawa na myama, hajali lolote wala chochote. Utamuona hamuogopi Mwenyezi Mungu, kwa kufanya maasi usiku na mchana. Tunamuomba Allah Subhaanahu wa Taala athibitishe nyoyo zetu juu ya twaa yake, na atulinde na machafu yote.