Find WhatsApp Channels
Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.
Channels & Posts for #juliusnyerereinternationalairport
Posts
Aviation Tanzania on Instagram: "Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Kupokea Ndege Kubwa za A380 Baada ya maboresho. Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Bertha Bankwa, ameeleza faida mbalimbali zitakazopatikana kufuatia ukarabati wa uwanja huo, ikiwa ni pamoja na kuanza kupokea ndege aina ya A380. Bi. Bertha ameyasema hayo jana, Februari 26, 2025, katika hafla ya utoaji wa fidia kwa wananchi wa eneo la Kipunguni waliopisha zoezi la upanuzi wa kiwanja hicho. Ameeleza kuwa maboresho hayo yanalenga kubadilisha hadhi ya uwanja huo kutoka Daraja la 4C kwenda Daraja la 4F, ambalo ndilo linalokidhi vigezo vya kupokea ndege za aina hiyo. Aidha, maboresho hayo yanatarajiwa kuchangia ongezeko la fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali zinazosaidia shughuli za uendeshaji wa uwanja huo. Miongoni mwa maeneo yatakayonufaika ni hoteli, kumbi, karakana za matengenezo ya ndege, pamoja na maghala ya kuhifadhi mizigo (cargo warehouses). . #airport #aviationtanzania #jnia #juliusnyerereinternationalairport #avgeek #tanzaniaairport #tanzaniaairportsauthority #tanzania🇹🇿 #aviationtanzaniaupdates #aviata"
https://www.instagram.com/p/DGkjGz0NUpb/?igsh=MWp3Z3BwbGZhcHVjMA== *Uwanja wa Ndege wa Kimataifa w...
Aviation Tanzania on Instagram: "Wananchi waliopisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere walipwa fidia ya Bilioni 20. Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imelipa fidia ya kiasi cha shilingi bilioni 20 kwa wakazi wa Mtaa wa Kipunguni, Jimbo la Segerea, Dar es Salaam,waliopisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA). Akizungumza wakati wa hafla ya ulipaji wa fidia, Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Abdul Mombokaleo, amesema kuwa malipo hayo ni sehemu ya awamu ya kwanza ya fedha zilizotengwa na serikali kwa ajili ya fidia kwa wananchi waliostahili. Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, ni moja kati ya viwanja viwili vikubwa vya kimataifa Tanzania bara, Julai 22, 2024 aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Bwana. Mussa Mbura alitangaza ongezeko la abiria wanaowasili katika uwanja wa JNIA kufikia 13% sawa na abiria milioni 3.8 hadi kufikia mwezi Julai 2024, ikilinganishwa na mwaka 2023 ambapo uwanja huo ulipokea jumla ya abiria milioni 2.8. Upanuzi na ukarabati wa uwanja huo, unatarajiwa kuongeza kasi ya matumizi yake na kuboresha zaidi huduma kwa abiria. . #airport #aviationtanzania #jnia #juliusnyerereinternationalairport #avgeek #tanzaniaairport #tanzaniaairportsauthority #tanzania🇹🇿 #aviationtanzaniaupdates #aviata"
https://www.instagram.com/p/DGi6PFFNGh1/?igsh=a29mbTU5MjZlcjJk *Wananchi waliopisha upanuzi wa uwan...