
Tanzanian Catholics Online
707 subscribers
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Sala kabla ya kuanza Kazi Tunakuomba ee Bwana uwe mwanzo na mwisho wa yote tunayofanya na tunayosema. Uyatangulie matendo yetu kwa mvuto wa neema yako na kuyaendeleza kwa msaada wako, ili sala na kazi zetu zote zianze pamoja nawe na kutimizwa pamoja nawe kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.


NOVENA YA ROHO MTAKATIFU SIKU YA NNE, JUMATATU Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina WIMBO WA ROHO MTAKATIFU Uje Roho (Sekwensia) 1. Uje Roho Mtakatifu, tuangaze toka mbingu, roho zetu kwa mwangao 2. Uje Baba wa maskini, uje mtoa wa vipaji, uje mwanga wa mioyo 3. Ee Mfariji mwema sana, ee Rafiki Mwanana, ewe raha mustarehe 4. Kwenye kazi u pumziko, kwenye joto burudisho, u mfutaji wa machozi 5. Ewe mwanga wenye heri, uwajaze waamini, neema yako mioyoni 6. Bila nguvu yako Wewe, mwanadamu hana kitu, kwake yote yana kosa 7. Osha machafuko yetu, panyeshee pakavu petu na kuponya majeraha 8. Ulegeze ukaidi, pasha moto ubaridi, nyosha upotovu wote 9. Wape waamini wako, wenye tumaini kwako, paji zako zote saba 10. Wape tuzo ya fadhila, wape mwisho bila hila, wape heri ya Milele. ROHO MTAKATIFU ANALIUNGANISHA KANISA “Atakapokuja huyu Roho wa kweli, atawaongoza kwenye ukweli wote” (Rej. Yn 16:13) Baada ya kusema hayo, Yesu aliinua macho yake kuelekea mbinguni akasema “Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha kazi uliyonipa niifanye. Naomba ili wote wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba Wewe ulinituma (Rejea Yn 17:4,21). Nasi twamuomba Mungu Mwenyezi alijalie Kanisa lake umoja wa kweli, awaunganishe Wakristo wa madhehebu yote katika zizi moja chini ya mchungaji mmoja. Popote duniani watu wengi, makundi kwa makundi wanavutwa na neema hiyo ya kuungana na kuufikia umoja wa Kanisa. Hata ndugu zetu waliotengana nasi wanazidi kukubali mwongozo wa Roho Mtakatifu na kutaka kurudi katika nyumba ya Baba na kuwa kundi moja chini ya mchungaji mmoja. Isitoshe, hata sasa tena twaweza kuona kwamba kwa namna fulani wamejiunga nasi katika Roho Mtakatifu, naye Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yao kumshuhudia hata kwa kumwaga damu yao. Tena katika hao ndugu zetu waliojitenga, Roho Mtakatifu analisha katika mioyo yao ile ya imani inayowaunganisha wafuasi wote wa Kristu. Tumwombe basi Mwenyezi Mungu atujalie hima huo umoja wa Kanisa lake tunaouania mno. 1. Ee Yesu Bwana wetu wewe umetuombea kwa Mungu Baba tuwe itu kimoja kama Wewe ulivyo kitu kimoja na Baba, Utujalie huo umoja, ili ulimwengu uone na kukiri kwamba ndiwe Bwana na Mkombozi wa watu wote. W. Twakuomba utusikie 2. Ee Yesu utujalie moyo wa kulishika neno lako kwa uaminifu, wala usituache kufuata njia zetu sisi wenyewe na kufarakana. W. Twakuomba utusikie 3. Ee Yesu uliye Mchungaji wetu mwema, ondoa ndani yetu ile tabia ya utengano, tupate kuwa sote kundi moja chini yako wewe uliye mchungaji wetu mmoja. W. Twakuomba utusikie 4. Ee Yesu, uliye Mchungaji mkuu, uwajalie wachungaji wetu wawe siku zote na upendo wa Jina lako, wasichoke kulichunga vema kundi lako hapa duniani na kuliweka pamoja lisitengane W. Twakuombaa utusikie 5. Ewe Roho Mtakatifu, uziangaze akili za watu wote, wapende siku zote kuishi kwa amani, umoja na mapendano W. Twakuomba utusikie 6. Ee Mungu, utufungulie ...... wa muungano wako wa kweli sisi tulio ndugu katika Bwana wetu Yesu Kristo. W. Twakuomba utusikie 7. Utujalie mapatano na amani, tudumu tumeungana katika familia zetu, katika Jimbo letu na katika nchi yetu yote. W. Twakuomba utusikie. TUOMBE; Ee Mungu, utuunganishe sisi kondoo wako tuliotawanyika, tuwe chini ya Mwanao mpenzi, tupate sote kuushiriki ule utawala wako wa kweli na haki, utawala wa neema na amani, utawala wa upendo wako. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu W. Amina LITANIA YA ROHO MTAKATIFU


*MASOMO YA MISA TAKATIFU,DOMINIKA YA PENTEKOSTE(08/06/2025)* *SOMO 1: Mdo 2:1-11* Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka. Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? Waparthi na Wamedi na Waelani, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu. *WIMBO WA KATI KATI Zab. 104:1, 24, 29-31, 34, (K) 30* (K) Waipeleka roho yako, Ee Bwana, Nawe waufanya upya uso wa nchi. Au: Aleluya. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Ee Bwana, jinsi yalivyo mengi matendo yako! Dunia imejaa mali zako. (K) Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao, Waipeleka roho yako, wanaumbwa, Nawe waufanya upya uso wa nchi. (K) Utukufu wa Bwana na udumu milele; Bwana na ayafurahie matendo yake. Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Mimi nitamfurahia Bwana. (K) *SOMO 2: 1Kor. 12:3b-7, 12-13* Hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. *SHANGILIO* Aleluya, aleluya, Uje Roho Mtakatifu, uzienee nyoyo za waamini wako uwatie mapendo yako. Aleluya. *INJILI: Yn 20:19-23* Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana. Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa. *----Tanzanian Catholics Online ---*


NOVENA YA ROHO MTAKATIFU SIKU YA TATU, JUMAPILI Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina WIMBO WA ROHO MTAKATIFU Uje Roho (Sekwensia) 1. Uje Roho Mtakatifu, tuangaze toka mbingu, roho zetu kwa mwangao 2. Uje Baba wa maskini, uje mtoa wa vipaji, uje mwanga wa mioyo 3. Ee Mfariji mwema sana, ee Rafiki Mwanana, ewe raha mustarehe. 4. Kwenye kazi u pumziko, kwenye joto burudisho, u mfutaji wa machozi. 5. Ewe mwanga wenye heri, uwajaze waamini, neema yako mioyoni 6. Bila nguvu yako Wewe, mwanadamu hana kitu, kwake yote yana kosa 7. Osha machafuko yetu, panyeshee pakavu petu na kuponya majeraha 8. Ulegeze ukaidi, pasha moto ubaridi, nyosha upotovu wote 9. Wape waamini wako, wenye tumaini kwako, paji zako zote saba 10. Wape tuzo ya fadhila, wape mwisho bila hila, wape heri ya Milele. ROHO MTAKATIFU ANATUFANYA KUWA MITUME Bwana alisema kwa kinywa cha nabii Yoeli; “Katika siku zile za mwisho asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, waume kwa wake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.... hata watumishi wenu watamiminiwa Roho wangu katika siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu." (Rejea Mdo.2:17-21) Siku ile ya Pentekoste, bada ya Roho Mtakatifu kulishukia Kanisa, mitume waliwakumbusha watu maneno haya ya nabii Yoeli na miaka mingi baadae, Petro aliwaandikia barua Wakristo wa kwanza akawaambia; kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile wakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu. Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumikia anapaswa kutumikia kwa nguvu aliyojaliwa na Mungu ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele (Rejea. Pet 4;10-11). Mtaguso wa Pili wa Vatikano ulitukumbusha jambo hilo hilo uliposema; “Roho Mtakatifu anayetakasa taifa la Mungu kwa njia ya Sakramenti amewapa waamini mapaji ya pekee na kumjalia kila mmoja kadiri apendavyo. Kwa hiyo kila mmoja amgawie mwenzake kadiri ya vipawa alivyopewa, awe mgawaji mwaminifu wa neema ya Mungu, alijenge kanisa zima katika upendo. Tunao wajibu wa kutumia vipawa tulivyojaliwa na Roho Mtakatifu kwa manufaa ya Kanisa zima na kwa faida ya watu wote. Tuunganike sote pamoja na wachungaji wote katika kazi hiyo ya utume. Tumuombe basi Roho Mtakatifu atusaidie kutumia vema vipawa vyake alivyotujalia. 1. Ewe Roho Mtakatifu uwape wakristo neema na nguvu za kutumia vema vipaji ulivyowajalia kwa ajili ya kujenga Kanisa lako popote duniani, kwa ajili ya wokovu wa watu wote. W. Twakuomba utusikie 2. Utujalie sisi sote mapaji yako saba, tupate kukutumikia kwa uchaji W. Twakuomba utusikie 3. Utujalie tuwe mitume wa kweli wa wenzetu, tushirikiane na wachungaji wetu katika huduma za kuwaongoza watu wote na kuwafikisha mbinguni W. Twakuomba utusikie. 4. Utujalie hekima na nguvu za kuwahudumia watu wote kwa mapendo ya kweli yasiyo na kinyume W. Twakuomba utusikie 5. Utujalie neema ya kumpenda Mungu kwa moyo wote na kuwapenda jirani zetu kama tunavyojipenda wenyewe W. Twakuomba utusikie 6. Utupe neema ya kulisikia neno lako na kulifuata, nayo mawazo yetu na matendo yetu yafuate daima mwongozo wako Mtakatifu W. Twakuomba utusikie 7. Uwazidishie mapaji yako wale wote wanaotumia vema vipawa vyao, uwarudishe na wale wanaotumia vibaya rehema zako W. Twakuomba utusikie TUOMBE; Ewe Roho Mungu ndiwe uliyewapa waamini vipawa vyako kwa kadiri unavyotaka. Utujalie tuyapokee na kuyatumia vema mapaji yako mengi kwa ajili ya utukufu wa Jina lako na kwa ajili ya wokovu wa watu wote. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. W. Amina LITANIA YA ROHO MTAKATIFU.


Wakati wa kwenda Kulala Ee Mungu wangu, pokea Roho yangu, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo aliyesulubiwa. Ninalala ili nipumzike. Unibariki Ee Bwana , na unikinge, uniepushe na Kifo cha Ghafla na kisichotarajiwa na hatari zote.Amina Mt.Yohane Paul wa Pili,Utuombee...🙏


*MASOMO YA MISA TAKATIFU,DOMINIKA YA PENTEKOSTE(08/06/2025)* *SOMO 1: Mdo 2:1-11* Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka. Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? Waparthi na Wamedi na Waelani, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu. *WIMBO WA KATI KATI Zab. 104:1, 24, 29-31, 34, (K) 30* (K) Waipeleka roho yako, Ee Bwana, Nawe waufanya upya uso wa nchi. Au: Aleluya. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Ee Bwana, jinsi yalivyo mengi matendo yako! Dunia imejaa mali zako. (K) Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao, Waipeleka roho yako, wanaumbwa, Nawe waufanya upya uso wa nchi. (K) Utukufu wa Bwana na udumu milele; Bwana na ayafurahie matendo yake. Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Mimi nitamfurahia Bwana. (K) *SOMO 2: 1Kor. 12:3b-7, 12-13* Hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. *SHANGILIO* Aleluya, aleluya, Uje Roho Mtakatifu, uzienee nyoyo za waamini wako uwatie mapendo yako. Aleluya. *INJILI: Yn 20:19-23* Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana. Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa. *----Tanzanian Catholics Online ---*


Sherehe ya Pentekoste: Roho Mtakatifu; Kanisa, Ushuhuda Na Kipindi Pasaka - | Vatican News - https://www.vaticannews.va/sw/church/news/2025-06/sherehe-pentekoste-roho-mtakatifu-kanisa-ushuhuda-kipindi-pasaka.html

*MASOMO YA MISA, DOMINIKA YA 6 YA PASAKA MWAKA C WA KANISA* *SOMO 1: Mdo. 15 :1-2, 22-29* Walishuka watu waliotoka Uyahudi wakawafundisha wale ndugu ya kwamba, Msipotahiriwa kama desturi ya Musa hamwezi kuokoka. Basi baada ya Paulo na Barnaba kushindana na watu hawa na kuhojiana nao sana, ndugu wakaamuru kwamba Paulo na Barnaba na wengine miongoni mwao wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee kwa habari ya swali hilo. Basi ikawapendeza mitume na wazee na kanisa lote kuwachagua watu miongoni mwao na kuwapeleka Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba; nao ni hawa, Yuda aliyeitwa Barsaba, na Sila, waliokuwa watu wakuu katika ndugu. Wakaandika hivi na kupeleka kwa mikono ya Mitume na ndugu wazee, kwa ndugu zetu walioko Antiokia na Shamu na Kilikia, walio wa Mataifa; Salamu. Kwa kuwa tumesikia ya kwamba watu waliotoka kwetu wamewasumbua kwa maneno yao, wakipotosha roho zenu, ambao sisi hatukuwaagiza; sisi tumeona vema, hali tumepatana kwa moyo mmoja, kuwachagua watu na kuwapeleka kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, watu waliohatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Basi tumewatuma Yuda na Sila, watakaowaambia wenyewe maneno hayo hayo kwa vinywa vyao. Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima, yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu. *WIMBO WA KATIKATI Zab. 67:1-5, 7, (K) 3* (K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru. Au: Aleluya. Mungu na atufadhili na kutubariki, Na kutuangazia uso wake. Njia yake ijulike duniani, Wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K) Mataifa na washangilie, Naam, waimbe kwa furaha, Maana kwa haki utawahukumu watu, Na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru. Mungu atatubariki sisi; Miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K) *SOMO 2: Ufu. 21:10-14, 22-23* Siku ile, mimi Yohana, Nilichukuliwa katika Roho mpaka mlima mnkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu; wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri; ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu, wenye milango kumi na miwili, na katika ile milango malaika kumi na wawili; na majina yameandikwa ambayo ni majina ya kabila kumi na mbili za Waisraeli. Upande wa mashariki milango mitatu; na upande wa kaskazini milango mitatu; na upande wa kusini milango mitatu; na upande wa magharibi milango mitatu. Na ukuta wa mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na katika ile misingi majina kumi na mawili ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo. Nami sikuona hekalu ndani yake, kwa maana Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake. Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo. *SHANGILIO: Yn 14 : 23* Aleluya, aleluya, Yesu alisema: Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake. Aleluya. *INJILI: Yn 14:23-29* Yesu aliwaambia wafuasi wake: Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka. Hayo ndiyo niliyowaambia wakati nilipokuwa nikikaa kwenu. Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia. Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga, Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda. mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba; kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi. Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, kusudi litakapotokea mpate kuamini. *Neno la Bwana.....Sifa kwako Ee Kristo.*


*MASOMO YA MISA TAKATIFU ,DOMINIKA YA SHEREHE YA KUPAA BWANA, MWAKA C(01/06/2025)* *SOMO 1: Mdo. 1:1-11* Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu. Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohane alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache. Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni. *WIMBO WA KATIKATI Zab. 47:1-2, 5-6, 7-8, (K) 5* (K) Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu. Au: Aleluya Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe, Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote. (K) Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu. Mwimbieni Mungu, naam, imbeni; Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni. (K) Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, Imbeni kwa akili. Mungu awamiliki mataifa, Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu. (K) *SOMO 2: Efe 1:17-23* Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote. *SHANGILIO: Mt. 28:19-20* Aleluya, aleluya, Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote. Aleluya. *INJILI: Lk 24:46-53* Yesu aliwaambia wafuasi wake, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya. Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu. Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki. Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni. Wakamwabudu; kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu. Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu. @Tanzanian Catholics Online ____
