
Bado nature visuals 📸
65 subscribers
About Bado nature visuals 📸
Step into the wild through the lens of Bado Nature Visuals – your exclusive window into Africa’s untamed beauty. From elusive wildlife to breathtaking landscapes, every image reveals nature’s raw elegance and untold stories. Follow for high-quality photography from Tanzania’s National Parks and beyond. Witness nature. Feel the moment. Stay inspired – and share the journey.
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Karibu kwenye safari ya 360°. Mto huu wa asili unazungumza kwa sauti ya utulivu, ukiwa katikati ya msitu wenye uhai wa kupumua. Angalia kila upande, jisikie kama upo hapa.


Elimu ya Leo: "Faida za kutembelea hifadhi za Taifa kama mtalii wa ndani 🇹🇿" 1. Kujifunza kuhusu urithi wa asili: Unapozuru hifadhi kama Serengeti, unajifunza kuhusu wanyama, mimea, na mazingira ambayo ni ya kipekee duniani. 2. Kusaidia uhifadhi: Kila tiketi unayonunua husaidia kulinda mazingira na wanyama walio hatarini kutoweka. 3. Fursa ya mapumziko ya kipekee: Ni njia ya kukwepa kelele za mijini na kupata utulivu wa asili. 4. Kujiendeleza kielimu na kitaaluma: Ni nafasi nzuri kwa wanafunzi, waandishi, wapiga picha na watafiti. 5. Kukuza uchumi wa jamii za jirani: Unapofanya utalii wa ndani, unasaidia familia nyingi zinazotegemea sekta hii.

_Usiku umetulia lakini mfalme halisi wa savanna ameamka_ - *FISI*

WAJUA? 🐒 Sokwe (Pan troglodytes) wanashiriki zaidi ya 98% ya vinasaba (DNA) na binadamu – wakiwa miongoni mwa viumbe wa karibu kabisa nasi katika mti wa maisha. Katika Mahale Mountains National Park, sokwe huishi kwenye familia zenye muundo wa kijamii, wakitumia zana kutafuta chakula — mfano kutumia vijiti kuopoa kupe kwenye mashina! 📍Picha hii ilipigwa ndani ya hifadhi ya Mahale, mkoani Kigoma, Tanzania.

*Simba dume...* *mfalme wa msitu.* Ngurumo yake si ya kutisha tu – ni ujumbe: hapa ni nyumbani. Watoto wake wapo salama, wakijifunza kutoka kwa _baba_ yao. Katika maisha ya kifalme, jukumu la _dume_ si kupambana tu, bali kulinda, kutunza, na kuhakikisha kizazi kinakuwa salama. Huyu si mnyama wa kawaida – ni *kiongozi* , ni mlinzi, ni baba. _Hii ndiyo hadithi ya simba... mlinzi wa kizazi._

*Anaangalia, anafikiri, anajifunza* ... 🐒 *Sokwe * ```ni``` ```miongoni mwa viumbe wenye akili kubwa. Wanaunda familia, wanatumia zana, na huonyesha hisia kama _binadamu_ — huzuni, furaha, hata wivu.``` ```Huyu alionekana akiwa ameshikilia mti, kimya, huku akiwaangalia wenzake — kama vile anajifunza au kufikiria hatua inayofuata . ``` *📍Mahale Mountains National Park* *© Bado Nature Visuals 2025*


*Upweke* *Nimesimama peke yangu* … Si kwa sababu wamenisahau, Bali kwa sababu nimejifunza kuchanua katika kimya. *> Naiona dunia ikipita mbele yangu.* Nayasikia maisha wakiwa mbali na mimi — Kicheko nisichokicheka, Nyimbo nisizoiimba pamoja nao. *> Lakini katika utulivu huu... nimemjua nafsi yangu* . Katika upepo unaovuma, nimesikia jina langu. > **Ninalia… si kwa uchungu* ,* Bali kwa uzuri ambao hakuna anayesimama kuuona. > *Wanafikiri niko mpweke* … Lakini ukweli ni kwamba, mimi ni huru. 📸Bado Nature Visuals 🖊️ M. Kupa 📍Mahale Mountains National Park.


Wanaponiangalia hivi, _Huenda wanajiuliza: 'Nani huyu anayethubutu kutupiga picha?'_ Lakini katika macho yao kuna hekima ya kizazi kilichopita 😂, waliobeba hadithi za usiku wa mwituni. *Fisi* si wa kuficha uso — wao ni wanamapinduzi wa *ekolojia* , wakiishi kwa mkakati wa pamoja usioeleweka kwa wengi. Wana jamii iliyo na mfumo wa kipekee kabisa: *jike* ndiye _kiongozi_ , na nguvu haipimwi kwa mwili tu bali kwa mafungamano. Wana *taya* zenye nguvu kuliko *Simba* , sauti za midomo zinazoitwa kwa majina, na uwezo wa kusoma _hisia_ za mmoja wao kwa _harufu_ . *Usiku wao ni mchana* — wakiwa mabingwa wa maamuzi kimya kimya. Hawa si ' _wapangaji wa mizoga' pekee,_ wao ni *wahandisi* wa mazingira, wakihakikisha hakuna kinachopotea. * *Fisi*, waliosimama mbele yangu, si wanyama tu. Ni mashahidi wa usiku, walinzi wa mizani ya pori. ............................................................................................. Share this post, kwa wingi uwezavyo 📸 Bado Nature visuals 📍 Tanzania National Park


Je ushawai fikiria kutembelea kwenye hifadhi za Tanzania?

Anaitwa *Yellow-billed stork* _(korongo domonjano_ ) Leo na simulizi fupi kuhusu ndege huyu 🪶 Nilitembea kwa saa kadhaa, bila lengo la kupiga picha. Nilitaka tu kukimbia kelele – za maisha, za watu, na za mawazo yangu mwenyewe. Nilipofika karibu na maji, nilimwona. Alisimama kama mchongaji wa kimya, akitazama upepo kwa heshima. Hakutetemeka, hakuniogopa, hakuwa na haraka. Kwa sekunde kadhaa, dunia ilisimama. Sauti ya maji ilinisamehe, jua lilinishika mkono, na yeye – ndege huyu mwenye mdomo wa njano – alinikumbusha kuwa kuishi haina maana kama hatujui kutulia. Nilipiga picha hii sio kwa ajili ya kumbukumbu ya macho, bali kumbukumbu ya moyo. Kwa mara ya kwanza, nilijisikia salama... porini. 📸 Bado Nature Visuals 📍 Lake Tanganyika Share this post
