Find WhatsApp Channels
Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.
Channels & Posts for #aviationupdate
Posts
Aviation Tanzania on Instagram: "Uwanja wa Ndege wa Arusha Kuanzisha Huduma Saa 24 Kuanzia Desemba. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameeleza kuwa, kuanzia mwezi Desemba 2025, Uwanja wa Ndege wa Arusha utaanza kutoa huduma kwa saa 24 kila siku. RC Makonda ameyasema hayo 17 Juni 2025 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu katika uwanja huo. Kwa sasa,wakandarasi wanaendelea na zoezi la kuweka taa za kuongozea ndege, hatua muhimu katika maandalizi ya kuufanya uwanja huo kutoa huduma zake Kwa saa 24. Aidha, serikali imepanga kupanua barabara ya kurukia na kutua ndege (runway) hadi kufikia urefu wa mita 500 na Ili kufanikisha hili, serikali inataraajia kuhamisha wakazi wa eneo la Magereza, ambalo lipo karibu na uwanja huo. #airport #tanzaniaairportsauthority #arushaairport #airportinfrastructure #runway #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/reel/DLAPeI3t18q/?igsh=MXU4NHBqcnA2ZW5zcA== *Uwanja wa Ndege wa Arusha Ku...
Aviation Tanzania on Instagram: "Shehena ya simu 1000 zilizoibiwa yakamatwa uwanja wa ndege zikipelekwa Afrika kaskazini. Polisi nchini Uingereza wamekamata shehena ya simu 1,000 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow, ikiwa ni sehemu ya oparesheni kubwa dhidi ya mitandao ya kihalifu inayojihusisha na wizi wa simu jijini London. Taarifa hiyo ilitolewa na Jeshi la Polisi la Jiji la London (Met Police) juni 3 mwaka huu, wakati wa kutoa ushahidi mbele ya Bunge la Uingereza kuhusu ongezeko la wizi wa simu katika mji huo mkuu, ambapo takribani simu 80,000 ziliripotiwa kuibwa katika mwaka 2024 pekee. Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Teknolojia na Takwimu za Kidijitali wa Met, Darren Scates, takwimu zinaonesha kuwa karibu asilimia 75 ya simu zinazoporwa huishia kupelekwa nje ya nchi, huku asilimia kubwa kati ya hizo zikipelekwa nchini Algeria na China/Hong Kong. Alifafanua kuwa Algeria na China kwa sasa ndio maeneo yanayopokea kwa kiwango kikubwa simu hizo. Alieleza kuwa miongoni mwa mafanikio ya hivi karibuni ni kukamatwa kwa zaidi ya simu 1,000 zilizoibwa katika Uwanja wa Heathrow, ambazo zilikuwa zikielekea Afrika Kaskazini. Hata hivyo, polisi hawakutaja tarehe halisi ya tukio hilo, wakieleza kuwa limefanyika miezi kadhaa iliyopita na uchunguzi bado unaendelea. Scates alisema kuwa utafiti uliofanywa unaonesha kuwa asilimia 80 ya simu zilizoibwa ni aina ya iPhone, na kila moja huwa na thamani ya mtaani ya kati ya paundi 300 hadi 400 Kwa ujumla, thamani ya simu zote zilizoibwa inakadiriwa kufikia paundi milioni 20. #airport #londonheathrowairport #airportinvestigation #northafrica #smartphones #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/p/DK6ZyrXtyoO/?igsh=MXA2aXVhcGwxYmU3MA== *Shehena ya simu 1000 zilizoibiw...
Aviation Tanzania on Instagram: "Jaribio la kwanza la kutua Kwa ndege lafanyika katika kiwanja cha ndege cha kimataifa, Msalato. Siku ya Jana Juni 13,2025, ndege aina ya Bombardier Q 400 inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Air Tanzania (ATCL), imetua kwa mafanikio katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya majaribio ya ufanisi wa kiwanja hicho kipya. Hili linakuwa ni jaribio la kwanza la kutua kwa ndege ya kibiashara katika kiwanja hicho ambacho kipo katika hatua za mwisho za maandalizi kabla ya kuanza rasmi kwa shughuli za usafiri wa anga. Kukamilika kwa kiwanja cha Ndege cha Msalato kutaiwezesha Tanzania kuwa na jumla ya viwanja vya ndege 62, ambapo vitatu kati yake vitakuwa ni viwanja vya kimataifa. #airport #tanzaniaairportsauthority #msalatointernationalairport #mia #atcl #q400 #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/reel/DK3wZNyNkpC/?igsh=eXBma3ExaXYwbDhh *Jaribio la kwanza la kutua Kwa n...
India’s aviation regulator mandates Air India to c...
India’s aviation regulator mandates Air India to complete power assurance checks on all Boeing 787-8...
BIG BREAKING: लखनऊ एयरपोर्ट से 4.5 महीने तक दिन मे...
BIG BREAKING: लखनऊ एयरपोर्ट से 4.5 महीने तक दिन में उड़ानें बंद! 📢 लखनऊ एयरपोर्ट पर 1 मार्च से 15 ...