Find WhatsApp Channels
Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.
Channels & Posts for #msalatointernationalairport
Posts
Aviation Tanzania on Instagram: "Jaribio la kwanza la kutua Kwa ndege lafanyika katika kiwanja cha ndege cha kimataifa, Msalato. Siku ya Jana Juni 13,2025, ndege aina ya Bombardier Q 400 inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Air Tanzania (ATCL), imetua kwa mafanikio katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya majaribio ya ufanisi wa kiwanja hicho kipya. Hili linakuwa ni jaribio la kwanza la kutua kwa ndege ya kibiashara katika kiwanja hicho ambacho kipo katika hatua za mwisho za maandalizi kabla ya kuanza rasmi kwa shughuli za usafiri wa anga. Kukamilika kwa kiwanja cha Ndege cha Msalato kutaiwezesha Tanzania kuwa na jumla ya viwanja vya ndege 62, ambapo vitatu kati yake vitakuwa ni viwanja vya kimataifa. #airport #tanzaniaairportsauthority #msalatointernationalairport #mia #atcl #q400 #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/reel/DK3wZNyNkpC/?igsh=eXBma3ExaXYwbDhh *Jaribio la kwanza la kutua Kwa n...
Aviation Tanzania on Instagram: "Kiwanja cha Ndege cha Msalato kuanza majaribio ya kuruka na kutua ndege mwezi Juni. Majaribio ya kuruka na kutua ndege katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato yanatarajiwa kuanza mwezi Juni 2025, ikiwa ni hatua muhimu kuelekea kukamilika kwa mradi huo mkubwa wa kimkakati unaotekelezwa jijini Dodoma. Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw.Abdul Mombokaleo, wakati wa ziara ya Waziri wa Ujenzi, Mh. Abdallah Ulega, aliyetembelea eneo hilo kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanja hicho. Bw.Mombokaleo amesema Kuwa maandalizi ya hatua hiyo yako mbioni kukamilika huku ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege ukiwa umekamilika kwa 89%. Katika ziara hiyo, Waziri Ulega ameagiza taasisi mbili muhimu TAA na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kushirikiana kwa karibu na kumsimamia kwa makini Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa jengo la abiria ili kuhakikisha ubora na muda wa mradi vinazingatiwa. Ulega alionya kuwa serikali haitatoa muda wa nyongeza kwa Mkandarasi huyo na endapo atashindwa kukamilisha mradi kwa wakati, atalazimika kuilipa serikali fidia kwa kuchelewesha utekelezaji. Hadi sasa, utekelezaji wa jumla wa mradi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato umefikia 53.9% na kukamilika kwa mradi huo kutaiwezesha Dodoma kuwa kitovu cha biashara, uchumi, na uwekezaji nchini Tanzania. #airport #mia #msalatointernationalairport #airportauthority #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/reel/DJ9vf3OsEgZ/?igsh=MXV1MWg2N2J3ZWpsaw== *Kiwanja cha Ndege cha Msalat...
Aviation Tanzania on Instagram: "Kaimu Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato,Clemence Jingu Mbaruku amebainisha chanzo cha ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji wa Dodoma, huku akieleza kuwa uwanja huo ulijengwa baada ya serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhamisha makao makuu ya nchi kutoka Dar es Salaam kuelekea katika mji wa Dodoma, huku lengo likiwa ni kuboresha uchumi na biashara katika mji huo. Imeelezwa kuwa kukamilika kwa uwanja huo kutaiweka Tanzania katika nafasi ya kipekee Afrika Mashariki kutokana na mifumo ya kisasa itakayowekwa katika barabara za kurukia na kutua ndege (runways) pamoja na jengo la abiria.Mifumo hii inatarajiwa kurahisisha ufanisi wa safari kwa abiria na kuimarisha ulinzi. Bwana Clemence Jingu Mbaruku ameeleza kuwa Uwanja huu utakuwa na mfumo wa taa za kuongozea ndege wa kisasa (Instrument Landing System - ILS) pamoja na mfumo wa ulinzi wa fensi yenye urefu wa kilomita 18. Runway yake ina upana wa mita 60 na urefu wa kilomita 3.6, ikiwezesha kuhudumia ndege kubwa za kimataifa. Mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato ulianza rasmi mwaka 2022 na hadi kufikia Januari 2025, mradi huo ulitajwa kufikia 83.5% kwa upande wa miundombinu na 51% kwa upande wa majengo, huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Novemba mwaka huu. . #airport #aviationtanzania #msalatointernationalairport #mia #avgeek #tanzaniaairport #tanzaniaairportsauthority #tanzania🇹🇿 #aviationtanzaniaupdates #aviata"
https://www.instagram.com/reel/DGdwhzxNM6G/?igsh=djNwaGJtZHI3MXp5 Kaimu Mkurugenzi wa Uwanja wa Nde...