
Wizara ya Afya Tanzania
231.4K subscribers
Verified ChannelAbout Wizara ya Afya Tanzania
Karibu kwenye ukurasa rasmi wa Wizara ya Afya Tanzania katika mtandao wa Whatsapp. Fuatilia ukurasa huu kwa habari mbalimbali za Sekta ya Afya #tunaboreshaafya #afyanimtaji
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

WANANCHI WAHAMASISHWA KUFIKA KATIKA HOSPITALI ZA WILAYA KUPATA HUDUMA ZA KIBINGWA Na. WAF, Iringa Wananchi Mkoani Iringa wahamasishwa kufika katika katika hospitali za wilaya ili kupata huduma za kibingwa kutoka kwa Madaktari Bingwa wa Dkt.Samia walioweka kambi ya siku tano (5). katika mkoa huo. Akizungumza wakati wa kuwapokea Madaktari Bingwa na wauguzi Bingwa 34 hao leo Juni 2, 2025 kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa , Mratibu wa Ushirikiano kati ya Serikali na sekta Binafsi Dkt.Credinus Mgimba amesema anamshukuru sana Mhe.Rais Dkt.Samia kwa kupeleka huduma hizo za kibingwa ili wananchi wa Mkoa wa Iringa na maeneo jirani wanufaike bila kusafiri umbali mrefu kufuata huduma na kutumia gharama kubwa. " Naishukuru pia Wizara ya Afya kuendelea kuratibu zoezi hilo pamoja na wataaam hao kwa uzalendo wao wa kufika katika mkoa huo kwa ajili ya kuhudumia wananchi sambamba na kuwajengea uwezo wataoa huduma katika maeneo yao ya kazi," amesema.Dkt. Mgimba Naye mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Bi.Upendo Mamchony amesema awamu ya kwanza ya kambi hizo za madaktari Bingwa wa Dkt.Samia ilikuwa na mafanikio makubwa kwani wagonjwa 2566 walipata huduma za kibingwa pamoja na upasuaji kwa wagonjwa 274 wakati waliopata Rufaa ni wagonjwa 238 ambao walipona na wanaendelea vizuri na shughuli zao. Hata hivyo mwakilishi huyo wa Wizara ya Afya amesema awamu hii wanatazamia kuhudumia zaidi ya wagonjwa 3000 mpaka 4000 Kambi hiyo ya siku tano katika mkoa wa Iringa imeanza Juni 2, 2025 na itahitimishwa Juni 6, 2025.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel akifuatilia kwa umakini wasilisho la Bajeti ya Wizara ya Afya ya mwaka wa fedha 2025/26 leo Juni 2, 2025, Bungeni jijini Dodoma inayowasilishwa na Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama.

TAASISI LIPENI MADENI YA MSD- WAZIRI MHAGAMA Na WAF, DODOMA Waziri wa Afya Mhe Jenista Mhagama ameziagiza Taasisi zote za Afya zinazodaiwa na Bohari ya Dawa (MSD) kuhakikisha zinalipa madeni kwa haraka ili MSD iweze kujiendesha kwa ufanisi. Waziri Mhagama ametoa agizo hilo Juni 03, 2025 Bungeni Dodoma wakati akijibu hoja za Wabunge waliotaka kuona MSD inaingia kwenye soko la ushindani kwa kushindana na washitiri wengine. โMadeni ambayo yapo chini ya fungu 52 (Wizara ya Afya) na mimi mwenyewe ambaye ni Waziri wa fungu 52 tayari tumeshaweka mkataba na Taasisi zote zilipe madeni ya MSD haraka sana,โ ameagiza Waziri Mhagama. Waziri Mhagama amesema kuwa tayari Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) wameshafanya vikao na MSD kwa ajili ya kuweka utaratibu mzuri wa Mamlaka zilizo chini ya OR-TAMISEMI kulipa madeni hayo. Mapema jana Juni 02, 2025 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI Mhe. Elibariki Kingu wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2024/25 alisema kuwa Kamati hiyo imebaini uwepo wa deni la Serikali kwa MSD lenye thamani ya Shilingi Bilioni 434.2. Mhe. Kingu aliishauri Serikali kuwa ni vyema ikalipa madeni hayo ili kuendelea kuulinda mnyororo wa ugavi na kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa utoshelevu. Kati ya Shilingi Bilioni 434.2 ambazo MSD inazidai Taasisi za afya, Shilingi Bilioni 46.4 ni kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma vilivyopo chini ya Wizara ya afya, Shilingi Bilioni 83.1 kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma vilivyopo chini ya OR-TAMISEMI na na Shilingi Bilioni 305 za miradi Misonge. Katika hatua nyingine, Waziri Mhagama amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuboresha utendaji kazi wa MSD kwa kuipa mtaji ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 150 tayari zimeshatolewa kwa MSD. โMSD iliwasilisha maombi ya mtaji wa kiasi cha Shilingi Bilioni 561, tayari Serikali imekwishatoa kiasi cha Shilingi Bilioni 150 kwa ajili ya kuboresha mtaji, Shilingi Bilioni 42 kwa ajili ya ujenzi wa maghala ya kuhifadhi bidha za dawa na hivi karibuni tunakwenda kupokea msaada wa zaidi ya Shilingi Bilioni 119 kutoka Serikali ya Watu wa Chinaโ amebainisha Waziri Mhagama akiwa anaelezea juhudi za Serikali kuiboresha MSD.

Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na Watumishi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kwa makini wasilisho la Bajeti ya Wizara ya Afya ya mwaka wa fedha 2025/26 leo Juni 2, 2025, katika ukumbi wa pembeni wa Bungeni jijini Dodoma

Wizara ya Afya leo Juni 04, 2025, imepokea ugeni kutoka Shirika la Evidence for Action, wenye nia ya kushirikiana na Wizara kwenye maeneo ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele, maji na usafi wa mazingira pamoja na lishe.

MIFUMO YA AFYA KUSOMANA KUANZIA NGAZI YA MSINGI HADI TAIFA โ WAZIRI MHAGAMA Na WAF- Dodoma. Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amewahakikishia Wabunge kuwa Serikali inakwenda kuboresha mifumo ya Sekta ya Afya inasomana kuanzia vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi hadi kufikia ngazi ya Taifa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa haraka pamoja na kuwapunguzia wananchi gharama za matibabu. Amesema hayo leo Juni 03, 2025 Bungeni Dodoma, wakati akijibu hoja za Wabunge kuhusu matumizi ya TEHAMA katika kuboresha upatikanaji wa huduma za afya. โHaiwezekani unatoka Songea unakwenda Njombe kwa matibabu unapima, ukienda Mbeya au Dar unapima, kitu ambacho kingeweza kurahisishwa kwa mifumo kusomana,โ amesema Waziri Mhagama na kuwahakikishia Wabunge kuwa Serikali itapambana ili kuwa na mifumo ambayo itakuwa ni suluhisho la uhaba wa watumishi pamoja na kupunguza gharama za matibabu.

WAZIRI MHAGAMA ALIOMBA BUNGE KUIDHINISHA TRILIONI 1.6 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA 2025/26 Na WAF - Dodoma Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amewasilisha Bungeni makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Afya Shilingi Trilioni 1.68 kwa ajili ya kutumika kutekeleza vipaumbele na afua mbalimbali kwenye mwaka wa fedha 2025/26. Waziri Mhagama amewasilisha bajeti hiyo, Bungeni jijini Dodoma Juni, 02, 2025 alipokuwa akiwasilisha makadirio ya Bajeti ya wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2025/26. Waziri Mhagama amesema Wizara ya Afya itaimarisha huduma za kinga dhidi ya magonjwa ya kuambukiza yakiwemo magonjwa ya milipuko, magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, magonjwa yasiyoambukiza na huduma za lishe kwa kutekeleza afua mbalimbali. Waziri Mhagama ameliambia Bunge kuwa suala la upatikanaji na ubora wa huduma za afya zinazotolewa katika ngazi zote kuanzia zahanati hadi taifa kwa kutekeleza afua ikiwa ni kuimarisha matumizi ya TEHAMA ikiwepo akili mnemba (Artificial Intelligence) pamoja na kuunganisha mifumo iweze kusomana. Waziri Mhagama ameongeza kuwa katika kipindi kijacho watajielekeza kwenye kuimarisha mifumo ya ugharamiaji wa huduma za afya nchini ikiwa ni pamoja na kuendelea na utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote kwa kutekeleza afua mbalimbali ikiwepo kutenga fedha kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya Sera za Kimataifa na ufadhili wa Sekta ya Afya. "Tutaimaridha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga kwa kutekeleza afua ikijumuisha ununuzi na usambazaji wa dawa muhimu za uzazi salama pamoja na dawa za uzazi wa mpango, dawa kinga za minyoo, dawa za kuongeza damu, dawa za malaria, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi," amesema Waziri Mhagama. Waziri Mhagama ameongeza kuwa bajeti hiyo imelenga upatikanaji na uendelezaji wa wataalam katika Sekta ya Afya kwa fani za kati, ubingwa na ubingwa bobezi kwa kutekeleza afua kama vile kutoa ufadhili wa mafunzo ndani na nje ya nchi kwa utaratibu wa seti kwa wataalam wa ngazi ya ubingwa na ubingwa bobezi na kufadhili mafunzo ya kada za kati za kimkakati. Kupitia fedha hizo trilion 1.6 Wizara itaimarisha huduma za matibabu ya ubingwa na ubingwa bobezi pamoja na kuimarisha tiba utalii nchini kwa kutekeleza afua kwa kuendelea kutoa huduma za matibabu ya ubingwa na ubingwa bobezi katika Hospitali ya Taifa, Hospitali maalum, Hospitali za Rufaa za Kanda na Hospitali za Rufaa za Mikoa pamoja na kuanzisha na kuimarisha huduma mpya kulingana na mahitaji. Eneo lingine litakalotiliwa mkazo ni kuendeleza na kusimamia afua za Tiba Asili na Tiba Mbadala kwa kutekeleza afua zinazojuisha kuuongeza Hospitali zinazotoa huduma jumuishi za Tiba Asili kutoka Hospitali za Rufaa za Mikoa 14 hadi 21. Waziri Mhagama amefafanua kwamba ili kuitekeleza Bajeti ya mwaka ujao watahakikisha wanaimarisha upatikanaji wa huduma za tiba dhidi ya magonjwa ya kuambukiza, magonjwa yasiyoambukiza na magonjwa ya mlipuko kwa kuimarisha uzalishaji wa viuadudu katika viwanda vya ndani. MWISHO