Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
May 25, 2025 at 05:52 AM
https://www.instagram.com/p/DKEKjixs9VT/?igsh=MWJ3N3J5dnlhMXBjZw== *Malaysia Airlines yazindua Airbus A330 yenye chapa ya timu ya Manchester United.* @malaysiaairlines imezindua ndege aina ya Airbus A330 iliyopakwa rangi na chapa ya klabu ya Manchester United, ikiwa tayari imefanyiwa majaribio ya kuruka angani. Ndege hiyo itatumiwa kuwasafirisha wachezaji wa Manchester United kutoka Kuala Lumpur kwenda Hong Kong kwa ajili ya mechi yao ya kirafiki dhidi ya timu ya wawakilishi wa Hong Kong, China, katika Uwanja wa Hong Kong Ijumaa ya tarehe 30 Mei 2025. Mechi hii ni sehemu ya ziara baada ya msimu ya Manchester United barani Asia, ambapo kabla ya kufika Hong Kong, watacheza dhidi ya ASEAN All Stars huko Kuala Lumpur, Malaysia, tarehe 28 Mei 2025. Kwa kusherehekea uzinduzi huu, mashabiki wanapata punguzo la hadi 50% kwa safari za kwenda Kuala Lumpur na Hong Kong. #airline #malaysiaairlines #manchesterunited #manufans #a330 #aviationlovers #aviationtanzania#aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates

Comments