Find WhatsApp Channels
Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.
Channels & Posts for #aviationtanzaniaupdates
Posts
Aviation Tanzania on Instagram: "Ndege ya Beechcraft King Air 90 yaanguka juu ya jengo la matengenezo ya ndege na kujeruhi watu wawili. Ndege aina ya Beechcraft King Air 90 imeanguka juu ya jengo la matengenezo ya ndege (hangar) Butler Avionics, katika Uwanja wa Ndege wa New Century Air Center, uliopo katika jimbo la Kansas, Marekani, na kujeruhi watu wawili waliokuwa ndani ya ndege hiyo. Ajali hiyo imetokea siku ya jana Juni 17,2025 wakati ndege hiyo ilipokuwa ikijaribu kutua,na badala ya kutua salama kwenye njia yake, ilitua moja kwa moja juu ya paa la jengo hilo. Waliokuwa ndani ya ndege hiyo ni rubani na mwanafunzi wa urubani ambao wameripotiwa kutoka Salama ndani ya ndege hiyo wakiwa na majeraha madogo na sasa wanapatiwa matibabu katika kituo cha afya kilicho karibu. #planecrash #beechcraftkingair #hangar #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/reel/DLCF-7ctTCw/?igsh=Y2hjcmc1YTZiNWE0 *Ndege ya Beechcraft King Air 90 ...
Aviation Tanzania on Instagram: "Air Tanzania is hiring for Cabin Crew and Captains. Air Tanzania Company Limited @airtanzania_atcl is inviting applications from qualified and experienced individuals to fill the following positions: Position: Captains (Q400) Number of Posts: 15 Position: Cabin Crew Number of Posts: 10 Interested candidates are encouraged to apply through the official recruitment portal: [https://recruitment.atcl.co.tz/](https://recruitment.atcl.co.tz/) The application deadline for all positions is 30 June 2025. #airline #airtanzania #aviationjobs #aviationcareer #airtanzania_atcl #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/p/DLAU9u6N4-M/?igsh=M2ZqN3ZvcXV6dDBq *Air Tanzania is hiring for Cabin Cr...
Aviation Tanzania on Instagram: "Uwanja wa Ndege wa Arusha Kuanzisha Huduma Saa 24 Kuanzia Desemba. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameeleza kuwa, kuanzia mwezi Desemba 2025, Uwanja wa Ndege wa Arusha utaanza kutoa huduma kwa saa 24 kila siku. RC Makonda ameyasema hayo 17 Juni 2025 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu katika uwanja huo. Kwa sasa,wakandarasi wanaendelea na zoezi la kuweka taa za kuongozea ndege, hatua muhimu katika maandalizi ya kuufanya uwanja huo kutoa huduma zake Kwa saa 24. Aidha, serikali imepanga kupanua barabara ya kurukia na kutua ndege (runway) hadi kufikia urefu wa mita 500 na Ili kufanikisha hili, serikali inataraajia kuhamisha wakazi wa eneo la Magereza, ambalo lipo karibu na uwanja huo. #airport #tanzaniaairportsauthority #arushaairport #airportinfrastructure #runway #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/reel/DLAPeI3t18q/?igsh=MXU4NHBqcnA2ZW5zcA== *Uwanja wa Ndege wa Arusha Ku...
Aviation Tanzania on Instagram: "Mmoja wa abiria waliosafiri Kwa Mara ya kwanza kutoka Nairobi hadi Arusha (WIL–ARK),Kwa kutumia ndege za shirika la @flightlinktz ameielezea safari hiyo kuwa ya haraka na yenye urahisi mkubwa. #Airlines #flightlink #newroute #routeexpansion #airlinepassenger #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/reel/DK_33PYtyzw/?igsh=cGpwY3lrY2lmdGU3 Mmoja wa abiria waliosafiri Kwa M...
Aviation Tanzania on Instagram: "Air Tanzania CEO speaks on EU Airspace Ban at AviaDev conference. During a panel discussion at the AviaDev Conference held in Zanzibar on June 12, 2025, the CEO of @airtanzania_atcl addressed the airline’s inclusion on the EU’s list of banned carriers. He outlined the airline’s strategy to overcome the situation, which includes working closely with consultants to implement a corrective action plan and introducing new routes from other destinations. According to a statement from the European Commission, aviation safety experts from EU member states identified significant shortcomings within Tanzania’s civil aviation oversight. The assessment revealed that the Tanzanian civil aviation authority had not sufficiently ensured compliance with international safety standards. Key concerns included an inadequate number of qualified personnel, weak oversight of flight operations and aircraft airworthiness, as well as failure to fully implement standards set by the International Civil Aviation Organization (ICAO). As a result, Tanzania was added to the EU Air Safety List, which now includes 169 airlines from 19 countries. Alongside Tanzania, Suriname was also newly added to the list, which already features nations such as Afghanistan, Libya, Nepal, and Sudan. #airline #airtanzania #euairspace #europe #airtanzania_atcl #aviation #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzania✈"
https://www.instagram.com/reel/DK_n6Bot_yD/?igsh=c2x3NDl1c2thMzJo *Air Tanzania CEO speaks on EU Ai...
Aviation Tanzania on Instagram: "Job opportunity at Coastal Air. @fly.coastal is currently hiring for Aviation security manager. Application Deadline: June 30, 2025. Submit your application, including a cover letter and CV to: [email protected] #airline #coastalair #aviationjobs #aviationcareer #flycoastal #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/p/DK9tTmtNVza/?igsh=MXI0OWs3YnVobHppaw== *Job opportunity at Coastal Air....
Aviation Tanzania on Instagram: "RC Makonda Ashuhudia Safari Mpya ya Flightlink Kutoka Nairobi Hadi Arusha. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, @baba_keagan , leo Juni 17,2025 ametembelea katika Uwanja wa Ndege wa Arusha na kushuhudia kwa mara ya kwanza safari mpya ya ndege ya shirika la Flightlink iliyoanzia Uwanja wa Ndege wa Wilson, jijini Nairobi, Kenya hadi uwanja wa ndege wa Arusha. RC Makonda alipata fursa ya kufanya mazungumzo na Mkuu wa Uendeshaji wa Flightlink Bw.Jameel Kassam kuhusu umuhimu wa safari hizo kwa mkoa wa Arusha na maendeleo ya sekta ya utalii na biashara. Safari hii mpya ya moja kwa moja kati ya Arusha (ARK) na Nairobi (WIL) ni ya kwanza kuanzishwa nchini Tanzania, safari ambayo hutumia muda wa Dakika 45. #Airlines #flightlink #newroute #routeexpansion #atr72 #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/p/DK9QCgltxDb/?igsh=NjlkaTJnc3dzN3dk *RC Makonda Ashuhudia Safari Mpya ya...
Aviation Tanzania on Instagram: "Ndege ya British Airways, Boeing 787-8 Dreamliner, yapata hitilafu ya kiufundi ikiwa njiani kuelekea India. Ndege ya abiria ya British Airways aina ya Boeing 787-8 Dreamliner iliyokuwa ikielekea Chennai, India, siku ya Jana Juni 15,2025 ililazimika kurejea Uwanja wa Ndege wa Heathrow jijini London baada ya kukumbwa na hitilafu ya kiufundi ikiwa angani. Ndege hiyo iliyokuwa ikifanya safari namba BA35, ilipaswa kuondoka Heathrow saa 6:40 mchana lakini ilichelewa na kuondoka saa 7:16 mchana (kwa saa za Uingereza) na Ilitarajiwa kufika Chennai saa 9:30 alfajiri (kwa saa za India). Kwa mujibu wa tovuti ya ufuatiliaji wa safari za ndege, Flightradar24, ndege hiyo ilibaki angani kwa karibu masaa mawili kabla ya kurejea salama Heathrow. Ingawa idadi kamili ya abiria waliokuwemo ndani ya ndege haijajulikana rasmi, video kadhaa zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha kuwa ndege hiyo ilikumbwa na tatizo kwenye moja ya sehemu za mabawa (flaps), hali iliyosababisha kurudi kwa dharura. Flightradar24 pia ilionesha kuwa ndege hiyo ilizunguka mara kadhaa angani kabla ya kutua. Katika taarifa iliyotolewa baadaye, British Airways ilithibitisha kuwa ndege hiyo ilitua salama na abiria wote pamoja na wafanyakazi walishuka salama bila matatizo yoyote. Hata hivyo, shirika hilo halikutoa maelezo ya kina kuhusu saa kamili ya kuondoka, muda halisi wa kuwa angani, au idadi ya watu waliokuwemo ndani. Tukio hili limetokea siku chache tu baada ya ajali mbaya ya ndege ya Air India Dreamliner huko Ahmedabad, India, ambapo watu 241 walifariki dunia tukio ambalo limezua taharuki kubwa kuhusu usalama wa ndege aina ya Dreamliner. Chanzo: First post #flightdiversion #boeing787dreamliner #britishairways✈️ #airindia #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/p/DK9MA9rtTap/?igsh=MXRkM2gzeDVsMnl3ZQ== *Ndege ya British Airways, Boein...
https://www.instagram.com/p/DK7j_6TNByQ/?igsh=MTlq...
https://www.instagram.com/p/DK7j_6TNByQ/?igsh=MTlqM21mcGV4M2M4ag== *Flightlink yazindua safari mpya...
Aviation Tanzania on Instagram: "Shehena ya simu 1000 zilizoibiwa yakamatwa uwanja wa ndege zikipelekwa Afrika kaskazini. Polisi nchini Uingereza wamekamata shehena ya simu 1,000 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow, ikiwa ni sehemu ya oparesheni kubwa dhidi ya mitandao ya kihalifu inayojihusisha na wizi wa simu jijini London. Taarifa hiyo ilitolewa na Jeshi la Polisi la Jiji la London (Met Police) juni 3 mwaka huu, wakati wa kutoa ushahidi mbele ya Bunge la Uingereza kuhusu ongezeko la wizi wa simu katika mji huo mkuu, ambapo takribani simu 80,000 ziliripotiwa kuibwa katika mwaka 2024 pekee. Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Teknolojia na Takwimu za Kidijitali wa Met, Darren Scates, takwimu zinaonesha kuwa karibu asilimia 75 ya simu zinazoporwa huishia kupelekwa nje ya nchi, huku asilimia kubwa kati ya hizo zikipelekwa nchini Algeria na China/Hong Kong. Alifafanua kuwa Algeria na China kwa sasa ndio maeneo yanayopokea kwa kiwango kikubwa simu hizo. Alieleza kuwa miongoni mwa mafanikio ya hivi karibuni ni kukamatwa kwa zaidi ya simu 1,000 zilizoibwa katika Uwanja wa Heathrow, ambazo zilikuwa zikielekea Afrika Kaskazini. Hata hivyo, polisi hawakutaja tarehe halisi ya tukio hilo, wakieleza kuwa limefanyika miezi kadhaa iliyopita na uchunguzi bado unaendelea. Scates alisema kuwa utafiti uliofanywa unaonesha kuwa asilimia 80 ya simu zilizoibwa ni aina ya iPhone, na kila moja huwa na thamani ya mtaani ya kati ya paundi 300 hadi 400 Kwa ujumla, thamani ya simu zote zilizoibwa inakadiriwa kufikia paundi milioni 20. #airport #londonheathrowairport #airportinvestigation #northafrica #smartphones #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/p/DK6ZyrXtyoO/?igsh=MXA2aXVhcGwxYmU3MA== *Shehena ya simu 1000 zilizoibiw...
Aviation Tanzania on Instagram: "Wote walinusurika Wakiwa Kwenye siti namba 11A: Mwanamuziki wa Thailand na Manusura wa ajali ya Air India. Msanii maarufu wa muziki nchini Thailand, Ruangsak Loychusak, ameibua hisia mpya za majonzi na mshangao baada ya kusimulia kuwa aliwahi kunusurika katika ajali mbaya ya ndege ya Thai Airways mwaka 1998 akiwa amekaa kwenye siti namba 11A – sehemu ileile ambayo Bw.Vishwash Kumar Ramesh, manusura pekee wa ajali ya ndege ya Air India, iliyotokea hivi karibuni, alikuwa ameketi. Ruangsak, ambaye alipata umaarufu mkubwa miaka ya 90 kwa jina la utani “Iron Bones”, alinusurika ajali ya ndege ya Thai Airways TG261 iliyotokea mnamo Disemba 11, 1998, wakati ndege aina ya Airbus ilipoanguka kwenye shamba la mpira huko Surat Thani, na kusababisha vifo vya watu 101. Akiwa ameketi katika kiti namba 11A, alinusurika kwa miujiza lakini aliishi na hofu ya kutumia usafiri wa anga kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi. Ruangsak alipata mshtuko baada ya kusikia kuwa Vishwash Kumar Ramesh, manusura pekee wa ajali ya ndege ya Air India, Boeing 787 Dreamliner iliyotokea tarehe 12 Juni 2025 huko Ahmedabad, India, naye alikuwa ameketi kwenye kiti namba 11A kabla ya ndege hiyo kuanguka katika bweni la chuo kikuu na kuua watu wote waliokuwemo isipokuwa yeye. Kupitia chapisho lake la hisia mitandaoni, Ruangsak alieleza kuwa taarifa hiyo ilimpa msisimko usio wa kawaida na kumfanya atafakari kwa kina namna maisha yalivyojawa na miujiza. Aidha, alitoa salamu za rambirambi kwa familia za wahanga wa ajali ya Air India, akisema kuwa kiti namba 11A sasa ni zaidi ya namba – ni alama ya matumaini na ushuhuda wa uhai katika mazingira ya maafa. #planecrash #survivor #planecrashsurvivor #airindia #boeing787dreamliner #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"
https://www.instagram.com/p/DK6TbhyNW8z/?igsh=MXhxbGh2ZTc5N2ZubA== *Wote walinusurika Wakiwa Kwenye...
Aviation Tanzania on Instagram: "Jaribio la kwanza la kutua Kwa ndege lafanyika katika kiwanja cha ndege cha kimataifa, Msalato. Siku ya Jana Juni 13,2025, ndege aina ya Bombardier Q 400 inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Air Tanzania (ATCL), imetua kwa mafanikio katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya majaribio ya ufanisi wa kiwanja hicho kipya. Hili linakuwa ni jaribio la kwanza la kutua kwa ndege ya kibiashara katika kiwanja hicho ambacho kipo katika hatua za mwisho za maandalizi kabla ya kuanza rasmi kwa shughuli za usafiri wa anga. Kukamilika kwa kiwanja cha Ndege cha Msalato kutaiwezesha Tanzania kuwa na jumla ya viwanja vya ndege 62, ambapo vitatu kati yake vitakuwa ni viwanja vya kimataifa. #airport #tanzaniaairportsauthority #msalatointernationalairport #mia #atcl #q400 #aviationupdate #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzanianews"
https://www.instagram.com/reel/DK3wZNyNkpC/?igsh=eXBma3ExaXYwbDhh *Jaribio la kwanza la kutua Kwa n...