Aviation Tanzania 🇹🇿  WhatsApp Channel

Aviation Tanzania 🇹🇿

80 subscribers

About Aviation Tanzania 🇹🇿

A channel dedicated to aviation news and information from Tanzania and around the globe.

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/20/2025, 8:09:56 AM

https://www.instagram.com/p/DGSZDO6NSTy/?igsh=MWJrdzNpdnR5dzd3aw== The Federal Aviation Administration (FAA) has found a safety risk in some Boeing 747 aircraft due to water leaks that could damage important electronic systems. This issue came to light after an incident where water from the aircraft's drinking water system leaked because of a faulty connection. The leak affected the engine warning and alert system, which provides critical information to pilots. To prevent future incidents, the FAA has issued a new safety rule requiring airlines to install protective barriers, such as shields and covers, over water pipes to stop leaks from reaching key electronics. This rule will take effect on March 21, 2025, and airlines in the U.S. must make the necessary changes to 178 affected aircraft, at an estimated cost of $1.2 million. These changes aim to ensure flight safety by keeping water away from essential flight control systems. #faa #waterleak #boeing747 #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates #aviatamedia #aviationcareer #aviationtanzania✈ #aviata #aviataupdates #aviatamedia #aviatatv

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/20/2025, 6:12:03 AM

https://www.instagram.com/p/DGSLowft_J8/?igsh=aWFleGZzZzBwMnht *Nchi 10 zinazo miliki ndege zenye umri mrefu zaidi barani Afrika* Unapopanda ndani ya ndege, huenda ikawa si rahisi kuwaza kuhusu umri wa ndege hiyo na muda ambao ndege hiyo imekuwa ikifanya safari zake, Lakini nyuma ya kila safari nzuri ya ndege, kuna hadithi yake. Umri wa ndege, unaopimwa tangu safari yake ya kwanza, huonyesha wastani wa miaka ambayo ndege imekuwa ikihudumu katika kundi la ndege za shirika husika. Kipimo hiki ni kiashiria muhimu kwa mashirika ya ndege na wasafiri, kikionyesha uwiano kati ya uboreshaji wa ndege, gharama za matengenezo, ufanisi wa mafuta, na hali ya abiria kwa ujumla. Duniani kote, wastani wa umri wa ndege za kibiashara hutofautiana sana. Baadhi ya nchi zina mashirika ya ndege yanayoendeshwa na ndege mpya kabisa, huku mashirika mengine yakiendelea kutumia ndege zenye miundo ya zamani. Ingawa ndege hizi za zamani zinaweza kukosa baadhi ya huduma zenye kustarehesha na ufanisi wa teknolojia mpya, bado zinatunzwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya usalama. Barani Afrika, mashirika mengi ya ndege hutumia baadhi ya ndege zenye umri mkubwa zaidi duniani. Hali hii inatokana na changamoto za kifedha, upatikanaji mdogo wa mtaji, na utegemezi wa ndege za zamani zilizonunuliwa kwa mara ya pili. Kwa mujibu wa takwimu za mtandao wa Planespotter, ndege za nchi ya Somalia zina wastani wa umri wa juu zaidi barani Afrika,huku wastani wake ukifukia miaka 33.9 inafuatiwa na nchi ya Sudan Kusini kwa wastani wa miaka 33, huku Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikiwa na ndege zenye wastani wa miaka 30.7. Chanzo- Business Insider #Airlines #sudanairways #somaliairlines #congoairways #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates #aviatamedia #aviationcareer #aviationtanzania✈ #aviata #aviat

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/20/2025, 4:30:03 PM

https://www.instagram.com/reel/DGTSKdqtRzp/?igsh=MTV0MnM2enlya2txZg== *Delta Airlines kuwalipa fidia ya $30,000 abiria waliopinduka na ndege Toronto.* Kampuni ya ndege ya Delta Air Lines imetangaza kuwalipa fidia ya dola 30,000 kila abiria aliyekuwa ndani ya ndege iliyopata ajali na kupinduka wakati wa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Pearson, Toronto, siku ya Jumatatu ya Februari 17,2025. Msemaji wa kampuni hiyo, amesema kuwa mpango wa fidia ni sehemu ya msaada wa kampuni kwa abiria waliokumbwa na ajali hiyo hiyo, akisisitiza kuwa fidia hiyo haitaathiri haki zao zozote za kisheria. Timu ya huduma ya Delta Care imekuwa ikiwasiliana na abiria ili kuwaarifu kuhusu fidia hiyo. Ndege hiyo,ilikuwa katika safari namba 4819, ilikuwa imebeba watu 80, wakiwemo abiria 76 na wafanyakazi wanne. Kufikia Jumatano asubuhi,abiria 20 kati ya abiria 21 waliokuwa wamelazwa hospitalini, walikuwa tayari wamepewa ruhusa ya kurudi nyumbani baada ya matibabu na hakuna vifo vilivyoripotiwa katika ajali hiyo. Mkurugenzi Mtendaji wa Delta Air Lines, Ed Bastian, akizungumza na chombo cha habari cha CBS Mornings, alisema kuwa ndege hiyo ilikuwa ikiendeshwa na kampuni tanzu ya Delta, Endeavor Air, na kuwa marubani walikuwa na uzoefu wa kutosha na mafunzo ya kukabiliana na hali yoyote. Bodi ya Usalama wa Usafiri nchini Canada (TSB) inaendelea kuchunguza chanzo cha ajali hiyo. Aidha, wachunguzi kutoka Bodi ya Kitaifa ya Usalama wa Usafiri ya Marekani (NTSB) na Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Shirikisho (FAA) pia wapo katika eneo la tukio kwa uchunguzi wa kina. . #planecrash #crj900 #toronto #deltaairlines #accident #safety #aircraft #aviationtanzania✈ #aviationta

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/20/2025, 9:51:34 AM

https://www.instagram.com/reel/DGSkOvFNIj5/?igsh=MWR3aTZ2ejBhNHlvNw== Daktari wa wanaanga nchini, @dr.nasranassor , ameeleza utaratibu rasmi kwa abiria mgonjwa anayepanga kusafiri kwa ndege. Alifafanua kuwa abiria hao wanapaswa kujaza fomu maalumu zinazopatikana katika mashirika mbalimbali ya ndege. Fomu hizo huwasaidia wahudumu wa ndege kutoa uangalizi wa karibu kwa mgonjwa katika kipindi chote cha safari yake. Tazama mahojiano haya kamili kwenye YouTube channel yetu, Aviation Tanzania, kwa kubonyeza kiungo kilichopo kwenye bio. #aviationmedicine #cabincrew #aviationcareer #aviation #aviationlovers #aviatamedia #aviationtanzaniaupdates #AviationTanzania✈

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/19/2025, 4:55:05 PM

https://www.instagram.com/reel/DGQvTcMNmCU/?igsh=MW5mN3V2ODVyc3BlNQ== Daktari wa Wanaanga Tanzania na muasisi wa @aerospace.medicaltz, @dr.nasranassor, ameeleza kuwa mtu yeyote aliyefanya upasuaji wa plastiki haruhusiwi kusafiri kwa ndege ndani ya siku saba, kwa sababu za usalama wa kiafya. Tazama mahojiano haya kamili kwenye YouTube channel yetu, Aviation Tanzania, kwa kubonyeza kiungo kilichopo kwenye bio. #aviationmedicine #cabincrew #aviationcareer #aviation #aviationlovers #aviatamedia #aviationtanzaniaupdates #AviationTanzania✈

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/20/2025, 12:58:19 PM

https://www.instagram.com/reel/DGS58Izt1Uy/?igsh=amVzaWJrMWpkbXQ5 *Ndege mbili zagongana angani, Abiria wa ndege moja wapoteza maisha, ndege nyingine wabaki salama.* Watu wawili wamepoteza maisha baada ya ndege mbili kugongana angani karibu na Uwanja wa Ndege wa Marana, Arizona, Februari 19,2025. Ajali hiyo ilihusisha ndege aina ya Cessna 1725 (N463ER) na Lancair 360 MK II (N3602M),ambazo ziligongana karibu na mwisho wa barabara ya ndege namba 12 huku kila moja ikiwa na abiria wawili ndani yake. Kufuatia ajali hiyo, Lancair ilianguka na kushika moto, na kusababisha vifo vya abiria wake wote wawili na ndege ya Cessna 1725 ilifanikiwa kutua salama, na abiria wote wawili wameripotiwa kuwa salama bila ya majeraha. Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Marekani (FAA) na Bodi ya Kitaifa ya Usalama wa Usafiri (NTSB) zinafanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo. . #accident #planecrash #cessna1725 #lancair #360mk #safety #aircraft #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates #aviatamedia #aviatatv

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/21/2025, 11:23:04 AM

https://www.instagram.com/p/DGVT70BtsK_/?igsh=MXFpazk1aWRkMWQzaA== *Ujenzi wa Uwanja wa Ndege Shinyanga Wagharimu Bilioni 44.8, kupokea ndege za Bombardier Q400.* Mradi wa ujenzi wa uwanja wa Ndege, Shinyanga umetajwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 44.8, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha miundombinu ya usafiri wa anga nchini. Mradi huu unajumuisha ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege yenye urefu wa mita 2,200, maingilio ya ndege (Taxiway), maegesho ya ndege (Apron), na jengo la abiria. Hayo yameelezwa katika ziara ya waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, ambaye alibainisha kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa mwanzoni mwa mwaka 2023 baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutoa maelekezo mahsusi ya kuhusu utekelezaji wake. Prof Mbarawa alifafanua kuwa ingawa mkataba wa mradi huo ulisainiwa mwaka 2017, utekelezaji wake ulikumbwa na changamoto mbalimbali zilizochelewesha kuanza kwake hadi aliporejea katika wizara hiyo mwaka 2022 na kupokea maelekezo ya moja kwa moja kutoka kwa Rais kuhusu umuhimu wa kuanza kwa miradi ya viwanja vya ndege vya Shinyanga, Katavi, Kigoma, na Tabora. Kwa mujibu wa Mhandisi wa Mradi kutoka Tanroads, Donatus Binemungu, kiwanja hicho kitakuwa na uwezo wa kupokea ndege za ukubwa wa aina ya Bombardier Q400. Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, alieleza kuwa kukamilika kwa uwanja huo kutachangia kukuza uchumi wa mkoa huo, hasa kupitia sekta ya usafirishaji wa madini yanayopatikana katika eneo hilo. . #airport #aviationtanzania #shinyanga #shinyangaairport #avgeek #tanzaniaairport #tanzaniaairportsauthority #tanzania🇹🇿 #aviationtanzaniaupdates #aviata

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/21/2025, 6:49:40 AM

https://www.instagram.com/p/DGU0hMiNbQT/?igsh=MXE4Z2I3YXF4b3l2cA== *Kenya Airways yajipanga kuongeza ndege 50 kwa kipindi cha miaka mitano.* Shirika la Ndege la Kenya Airways (KQ) limetangaza mpango wa kuongeza zaidi ya ndege 50 katika kipindi cha miaka mitano ijayo kama sehemu ya mkakati wa kuimarisha shirika hilo. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo Bw.Allan Kilavuka katika mahojiano na Shirika la habari la NTV na kuweka wazi kuwa lengo la shirika hilo ni kuimarisha uwezo wake wa uendeshaji kutoka hadhi ya sasa ya "sub-scale" hadi kiwango endelevu kitakachowezesha usimamizi mzuri wa gharama za uendeshaji. Hata hivyo, juhudi za kutafuta mwekezaji wa kimkakati kwa sasa zimesitishwa ambapo serikali pamoja na wawekezaji wa shirika hilo, wameomba muda zaidi wa kupata mshirika sahihi wa kibiashara. Wakati huu, KQ inazingatia kuongeza uwezo wa kuhudumia abiria kwa kuongeza ndege kupitia ukodishaji wa muda mrefu. Katika hatua nyingine, Kenya Airways imeingia makubaliano ya kukodi ndege kutoka kampuni ya Dubai Aerospace Enterprise (DAE). Mikataba hii ya ukodishaji wa ndege kwa kawaida huchukua kati ya miaka 8 hadi 12, jambo linalowanufaisha pande zote mbili kwa kuwa uwekezaji huo ni wa muda mrefu. Shirika hilo limeeleza kuwa gharama ya kukodisha kila ndege kwa mwezi inakadiriwa kuwa kati ya Dola za Kimarekani 250,000 hadi 400,000. Licha ya mikataba hiyo, Kenya Airways bado inaendelea kufuatilia uwezekano wa kupata mtaji wa ziada ili kuendeleza mkakati wake wa kupanua Shirika hilo huku lengo likiwa ni kuimarisha idadi ya ndege zake na kuboresha nafasi yake katika soko la usafiri wa anga barani Afrika na kimataifa. Chanzo- @ntvkenya . #Airlines #kenyaairways #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates #aviatamedia #aviationcareer #aviationtanzania✈ #aviata #aviat

Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/19/2025, 7:08:40 PM

https://www.instagram.com/p/DGQ_ucpNAe5/?igsh=MWUzZ3QxYWExcjgwdg== *Mjasiriamali, Hashim Walters aazimia Kuifanya Spirit Airlines kuwa ya wamarekani weusi* Kutoka New Orleans, Louisiana,nchini Marekani,Hashim Walters, mjasiriamali mwenye umri wa miaka 29, ameanzisha rasmi kundi la biashara linaloitwa The Latimer Group,kwa lengo la kuinunua Spirit Airlines, chapa maarufu ambayo kwa sasa inayokabiliwa na changamoto kubwa za kifedha. Walters amesema kuwa, dhamira yake ni kuwawezesha viongozi wa kiuchumi wa Kiafrika nchini Marekani, kwa kuunda shirika pekee la ndege la kibiashara linalomilikiwa na wamarekani weusi nchini Marekani. . #Airlines #spiritairlines #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates #aviatamedia #aviationcareer #aviationtanzania✈ #aviata #aviat

Image
Aviation Tanzania 🇹🇿
Aviation Tanzania 🇹🇿
2/19/2025, 3:57:35 PM

https://youtu.be/kSVsRfPn_mI?si=ESErQHGKc1-4UHFp

Link copied to clipboard!