
Aviation Tanzania 🇹🇿
May 29, 2025 at 09:33 AM
https://www.instagram.com/reel/DKO3_5SMbyV/?igsh=cWx0NjRwd3NhdWl0
*Tazama jinsi “drones”zinavyotumika kupulizia dawa za kuua wadudu shambani Wilayani Igunga.*
Mbali na matumizi ya kawaida ya ndege nyuki (drones) kwa ajili ya kurekodi picha na video katika uzalishaji wa maudhui, teknolojia hii pia inatumika kwa matumizi mengine muhimu.
Katika Wilaya ya Igunga, ndege nyuki (drones) zinatumika katika shughuli za kilimo hasa katika zoezi la kumwaga dawa za wadudu hatari kwa mazao.
Drone hizi zimetajwa kurahisisha zoezi la umwagiliaji wa dawa, ambapo inatumia dakika sita kumwagilia shamba la hekari moja, tofauti na awali ambapo wakulima walitumia muda mrefu zaidi kukamilisha zoezi hilo huku wakikumbana na changamoto kadhaa ikiwemo wadudu kuhamia eneo ambalo halijapuliziwa dawa.
Zoezi hili la kupulizia dawa ya wadudu mashambani sehemu ya mradi wa Build a better Tomorrow (BBT) uliochini ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
#drone #dronepilot #aviationinagriculture #bbt #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates