
Aviation Tanzania 🇹🇿
June 7, 2025 at 06:00 PM
https://www.instagram.com/p/DKm9B4wNwpQ/?igsh=MWhubHIxdXJnM2M3NQ==
*Flightlink yashiriki katika maonyesho ya Karibu Kilifair Arusha.*
Flightlink yashiriki katika maonyesho ya Karibu Kilifair Arusha.
Shirika la ndege la @flightlinktz , limeshiriki katika maonyesho ya kibiashara na Utalii ya Karibu Kilifair Kwa mwaka 2025.
Maonyesho hayo yaliyozinduliwa siku ya Jana Juni 6,2025 yalihudhuriwa na mgeni rasmi, Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mh.Dotto Biteko, yanafanyika katika viwanja vya Magereza jijini Arusha na yanatarajia kuhitimishwa siku ya kesho Juni 08,2025.
Zaidi ya makampuni 500 kutoka Afrika mashariki yamepata fursa ya kuonyesha bidhaa na huduma zao katika maonyesho hayo Kwa mwaka huu, maonyesho ambayo yanatazamiwa kukuza zaidi sekta ya utalii wa ndani na nje ya nchi.
Flightlink imepata fursa ya kuonyesha na kutangaza zaidi huduma ya safari zake ikiwemo safari mpya zinazotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni zikiwemo safari za ndani na nje ya nchi.
Endelea kutufuatilia Kwa habari mbalimbali kuhusu maonyesho ya Karibu Kilifair 2025.
#exhibition #airline #flightlink #newroutes #routeexpansion #ys #kilifair2025 #aviationtanzaniaupdates #aviationtanzania✈