
Aviation Tanzania 🇹🇿
June 13, 2025 at 11:13 AM
https://www.instagram.com/p/DK1r4EfNtRu/?igsh=bzQwbGUwM2R6a2l1
*Wanafunzi wa Shule ya Alpha wapelekwa Kenya kupata mafunzo ya urubani wakati wa likizo.*
Shule ya Sekondari ya @alphaschoolstz imewapeleka wanafunzi wake nchini Kenya kwa ajili ya kupata mafunzo ya urubani katika kipindi cha likizo ya mwezi wa sita.
Hii ni sehemu ya mwendelezo wa somo la Aviation lililoanzishwa na shule hiyo mwezi Mei 2022 kwa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza hadi cha Sita.
Kupitia programu hii ya kipekee, wanafunzi hujifunza kwa vitendo urushaji wa ndege pamoja na kupata uzoefu na ujuzi wa kutosha katika sekta ya usafiri wa anga. Mafunzo haya yanajumuisha vipindi vya nadharia darasani pamoja na mazoezi ya kurusha ndege yanayofanyika moja kwa moja kwa vitendo.
Programu hii inalenga kuwajengea wanafunzi msingi bora wa taaluma ya urubani na kuwaandaa kwa fursa mbalimbali ndani ya sekta ya anga, huku wakiendelea kufuata ndoto zao za kuwa marubani wa baadaye.
#aviationtraining #alphaschool #futureaviators #aviationcareer #futurepilots #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates