Find WhatsApp Channels

Discover the best WhatsApp channels for news, entertainment, education and more. Our powerful search helps you find exactly what you're looking for.

Channels & Posts for #aviationcareer

Posts

Aviation Tanzania on Instagram: "Air Tanzania is hiring for Cabin Crew and Captains. Air Tanzania Company Limited @airtanzania_atcl is inviting applications from qualified and experienced individuals to fill the following positions: Position: Captains (Q400) Number of Posts: 15 Position: Cabin Crew Number of Posts: 10 Interested candidates are encouraged to apply through the official recruitment portal: [https://recruitment.atcl.co.tz/](https://recruitment.atcl.co.tz/) The application deadline for all positions is 30 June 2025. #airline #airtanzania #aviationjobs #aviationcareer #airtanzania_atcl #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DLAU9u6N4-M/?igsh=M2ZqN3ZvcXV6dDBq *Air Tanzania is hiring for Cabin Cr...

Aviation Tanzania on Instagram: "Job opportunity at Coastal Air. @fly.coastal is currently hiring for Aviation security manager. Application Deadline: June 30, 2025. Submit your application, including a cover letter and CV to: [email protected] #airline #coastalair #aviationjobs #aviationcareer #flycoastal #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DK9tTmtNVza/?igsh=MXI0OWs3YnVobHppaw== *Job opportunity at Coastal Air....

https://www.instagram.com/p/DK7j_6TNByQ/?igsh=MTlq...

https://www.instagram.com/p/DK7j_6TNByQ/?igsh=MTlqM21mcGV4M2M4ag== *Flightlink yazindua safari mpya...

Aviation Tanzania on Instagram: "Precision Air yatembelea Kituo cha watoto Cornel Ngaleku, kumuenzi muanzilishi wa Shirika hilo. Shirika la ndege la @precisionairtz limepata fursa ya kutembelea Kituo cha Watoto cha Cornel Ngaleku na kutoa msaada wao wa upendo kwa watoto waliopo kituoni hapo. Kupitia ujumbe wake rasmi, shirika hilo limeeleza kuwa, ziara hiyo pia imefanyika Kama namna ya kumuenzi mwanzilishi wa shirika hilo, marehemu Michael Shirima, ambaye ndoto na maono yake bado yanaendelea kuwa dira ya huduma na mshikamano wa kijamii. Kupitia tukio hilo, Precision Air imeeleza kuguswa na furaha iliyosambaa kwenye nyuso za watoto hao, jambo linalothibitisha nguvu ya huruma na mshikamano wa jamii. #Airlines #pw #precisionair #youarewhywefly #aviationlovers #aviationcareer #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DK2aM52tiI9/?igsh=MncyMDFtYjBhMzd1 *Precision Air yatembelea Kituo cha ...

Aviation Tanzania on Instagram: "Mkuu wa uendeshaji wa shughuli za shirika la ndege la Flightlink, @jfk_1 ameeleza Lengo la ushiriki wa kampuni ya @flightlinktz katika mkutano wa kimaendeleo katika sekta ya Anga wa Aviadev na faida ambazo shirika hilo limezipata tangu liliposhiriki katika mkutano huo Kwa Mara ya kwanza mwaka 2024 nchini Namibia. #Airlines #flightlink #aviadev #aviationcareer #aviadevafrica #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/reel/DK19N-Ttxz7/?igsh=OGp0cHhzM2lvZGhz Mkuu wa uendeshaji wa shughuli za...

Aviation Tanzania on Instagram: "Wanafunzi wa Shule ya Alpha wapelekwa Kenya kupata mafunzo ya urubani wakati wa likizo. Shule ya Sekondari ya @alphaschoolstz imewapeleka wanafunzi wake nchini Kenya kwa ajili ya kupata mafunzo ya urubani katika kipindi cha likizo ya mwezi wa sita. Hii ni sehemu ya mwendelezo wa somo la Aviation lililoanzishwa na shule hiyo mwezi Mei 2022 kwa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza hadi cha Sita. Kupitia programu hii ya kipekee, wanafunzi hujifunza kwa vitendo urushaji wa ndege pamoja na kupata uzoefu na ujuzi wa kutosha katika sekta ya usafiri wa anga. Mafunzo haya yanajumuisha vipindi vya nadharia darasani pamoja na mazoezi ya kurusha ndege yanayofanyika moja kwa moja kwa vitendo. Programu hii inalenga kuwajengea wanafunzi msingi bora wa taaluma ya urubani na kuwaandaa kwa fursa mbalimbali ndani ya sekta ya anga, huku wakiendelea kufuata ndoto zao za kuwa marubani wa baadaye. #aviationtraining #alphaschool #futureaviators #aviationcareer #futurepilots #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DK1r4EfNtRu/?igsh=bzQwbGUwM2R6a2l1 *Wanafunzi wa Shule ya Alpha wapelek...

Aviation Tanzania on Instagram: "The CEO of @fly.ethiopian , Mr.Mesfin Tasew Bekele, participates in a panel discussion on the development of Africa’s aviation sector during the AviaDev 2025 conference in Zanzibar. #Airlines #ethiopianairlines✈️ #aviadev #aviationcareer #aviadevafrica #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DK1SCkONk7a/?igsh=MXhwNThieWV6bDF2dQ== The CEO of @fly.ethiopian , Mr.M...

Aviation Tanzania on Instagram: "Zanzibar yapiga hatua mpya kuelekea kuanzisha Shirika la ndege la Kitaifa. Zanzibar iko katika mazungumzo na wawekezaji mbalimbali kuhusu mpango wa kuanzisha shirika lake la ndege la kitaifa hatua inayolenga kuboresha muunganiko wa visiwa hivyo na kukuza sekta ya utalii. Tangazo hilo lilitolewa Jumatatu katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kilichofanyika Chukwani, ambapo Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mheshimiwa Nadir Abdulatif Yussuf, alieleza kuwa serikali ya Zanzibar tayari iko katika mazungumzo na shirika la ndege la EgyptAir kuhusu mpango wa kushirikiana kuanzisha shirika hilo jipya. Mheshimiwa Yussuf alibainisha kuwa majadiliano na EgyptAir yanaendelea vizuri, na kwamba pande zote mbili tayari zimefikia makubaliano ya awali ya kuweka mfumo wa ushirikiano kwa ajili ya kuanzisha shirika la ndege la Zanzibar. Kauli hiyo imetolewa kufuatia hoja iliyotolewa na Mwakilishi wa Mtambwe, Dkt. Mohamed Ali Suleiman, ambaye aliitaka serikali kuangalia kama huu ndio wakati muafaka wa kutekeleza mpango wa muda mrefu wa kuwa na shirika la ndege litakalotambulika kitaifa kutoka Zanzibar. Ikiwa mpango huu utakamilika, utaiweka Zanzibar katika nafasi nzuri ya kushindana kikanda katika sekta ya usafiri wa anga, huku ukitarajiwa pia kuongeza idadi ya watalii wanaofika visiwani kwa urahisi zaidi. Chanzo: The Citizen #Airlines #zanzibar #newairline #aviationcareer #aakia #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DKuu_o1tuFY/?igsh=bWw3ZXN5ampsMnB2 *Zanzibar yapiga hatua mpya kuelekea...

Aviation Tanzania on Instagram: "Katika maonyesho ya @kilifair 2025, Mkurugenzi wa Shirika la Ndege la @flightlinktz , @munawerdhirani ameeleza namna shirika hilo lilivyojipanga kuongeza safari za ndani na nje ya nchi. Safari hizo ni pamoja na zile kati ya Uwanja wa Ndege wa Arusha na uwanja wa ndege wa Wilson zitakazozinduliwa tarehe 15 Juni 2025, pamoja na safari kati ya Zanzibar na Jomo Kenyatta zitakazoanza tarehe 1 Julai 2025. Aidha, Flightlink imepanga kuanzisha safari kati ya Mwanza na Kilimanjaro, zitakazozinduliwa ndani ya mwezi Julai. #Airlines #routeexpansion #flightlink #aviationlovers #aviationcareer #atr72500 #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/reel/DKoSH0Pt-2f/?igsh=MTd5YnNsd204dnNyZw== *Flightlink yapanga kuanzisha...

Aviation Tanzania on Instagram: "Job Opportunities at Air Tanzania @airtanzania_atcl is hiring, The national carrier has announced multiple job vacancies for qualified and passionate professionals to join its growing team in the aviation industry. Below are the available positions: Aircraft Maintenance Engineer II – 8 posts Planning & Development Engineer II – 22 posts Aircraft Technician II – 30 posts Aviation Security Assistant II – 4 posts Application deadline: June 17, 2025 Apply now via: [https://recruitment.atcl.co.tz/](https://recruitment.atcl.co.tz/) #airline #airtanzania #aviationjobs #aviationcareer #airtanzania_atcl #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DKeCfYAtSIt/?igsh=MmRubDV2NnVldnh3 *Job Opportunities at Air Tanzania* ...

Aviation Tanzania on Instagram: "TAA yatangaza kuanza Kwa safari mpya za shirika la ndege la Flightlink. Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania @tanzaniairports imetangaza kuanza kwa safari mpya za anga za shirika la ndege la @flightlinktz kati ya miji ya Arusha na Nairobi, kuanzia tarehe 15 Juni 2025. Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na TAA, Flightlink itaanzisha safari ya kila siku kutoka Arusha kwenda Nairobi, ikiwa ni hatua muhimu katika kuboresha huduma za usafiri wa anga katika ukanda wa Kaskazini mwa Tanzania. Katika maandalizi ya safari hizo,TAA ikishirikiana na Ofisi ya Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, iko mbioni kukamilisha mfumo wa upokeaji na upangaji wa maafisa wa uhamiaji katika Uwanja wa Ndege wa Arusha ili kuhakikisha safari hizo zinafanyika kwa ufanisi. TAA imesisitiza kuwa inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya usafiri wa anga kuhakikisha huduma bora kwa abiria na kuwezesha maoni kutoka kwa watumiaji wa viwanja vyake ili kuboresha huduma zaidi. #Airlines #flightlink #aviationlovers #aviationcareer #ys #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdates"

https://www.instagram.com/p/DKZPgzoMsxD/?igsh=YTdveW5ndnF5ZnRt *TAA yatangaza kuanza Kwa safari mpy...

Aviation Tanzania on Instagram: "TCAA na Idara ya uhamiaji wasaini mpango wa kubadilishana taarifa Kidijitali. Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania @officialtcaa na Idara ya Uhamiaji @uhamiajitz leo Mei 27,2025 wameingia katika makubaliano rasmi ya kushirikiana katika kubadilishana taarifa kwa njia ya kidijitali, hatua inayolenga kuimarisha usalama wa anga, kuongeza ufanisi wa huduma, na kuboresha takwimu muhimu, hususan katika sekta ya utalii. Makubaliano hayo yamefanyika jijini Dodoma katika makao makuu ya Idara ya Uhamiaji na kushuhudiwa na viongozi waandamizi kutoka taasisi zote mbili,yakisiniwa na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Salim Msangi, na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Bi. Anna Makakala. Bw. Msangi alisema kuwa mpango huu umeanzishwa katika kipindi mwafaka ambapo matumizi ya teknolojia ya kisasa yazidi kuongezeka Kwa kasi duniani. If Alieleza kuwa kupitia ushirikiano huo, TCAA itaongeza ufanisi wa operesheni zake, kuimarisha usalama wa anga na kusaidia katika udhibiti bora wa wageni wanaoingia na kutoka nchini kupitia viwanja vya ndege. Kwa upande wake, Kamishna Jenerali Makakala alibainisha kuwa Idara ya Uhamiaji itaendeleza ushirikiano wa karibu na TCAA ili kuhakikisha kuwa taarifa za abiria na safari za anga zinawasilishwa kwa usahihi na kwa wakati. Mpango huu pia unatarajiwa kuboresha ukusanyaji wa takwimu za wageni wanaoingia nchini, jambo litakalosaidia katika kupanga mikakati madhubuti ya kukuza sekta ya utalii na uchumi wa taifa kwa ujumla. #tcaa #tanzaniacivilaviationauthority #aviationcareer #aviationtanzania✈ #aviationtanzaniaupdates #aviata #aviataupdate"

https://www.instagram.com/p/DKKWl8mMhJF/?igsh=emt0NGtlZG1oMTZi *TCAA na Idara ya uhamiaji wasaini m...