
NMB Bank Plc
276.7K subscribers
Verified ChannelAbout NMB Bank Plc
Welcome to our Official NMB Bank WhatsApp Channel. Stay active with the latest updates, banking tips, exclusive promotions, and valuable insights directly from us.
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Maadhimisho ya Miaka 10 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yamehitimishwa rasmi leo na Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Peter Msofe. Uwakilishi wa Benki ya NMB umeongozwa na Bi. Josina Njambi, Mkuu wa Kitengo cha Ubunifu, aliyeambatana na baadhi ya wawakilishi wa Benki na wadau mbalimbali wa maendeleo ya teknolojia. Kama Benki, tutaendelea kuwekeza katika ubunifu kwa kuifikia jamii ya vijana kupitia masuluhisho ya kidijitali, program za kukuza vipaji, na ushirikiano na taasisi za elimu, ili kuandaa kizazi cha kesho chenye uwezo wa kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa njia bunifu. #NMBKaribuYako

📍 Pwani Miaka mitatu mfululizo, Benki ya NMB imedhamini na kushiriki maonesho ya kimataifa ya mifugo na ufugaji bora ya Tri-Nations Livestock Expo 2025, yanayowakutanisha wadau katika mnyororo wa thamani katika sekta ya Ufugaji kutoka ndani na nje ya nchi. Katika maonesho haya, wafugaji kutoka nchi mbalimbali wameshiriki katika kuonesha mifugo yao na wamejifunza mbinu bora za ufugaji. Maonesho haya yamefunguliwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti na uwakilishi wa Benki umeongozwa na Mkuu wetu wa Idara ya Kilimo Biashara, Nsolo Mlozi aliyeambatana na Mkuu wa Idara ya Bima, Martine Massawe, Meneja wetu wa Kanda ya Dar es Salaam, Seka Urio, pamoja na wafanyakazi wengine wa Benki. #NMBKaribuYako


Uwakilishi wa Benki ya NMB ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wetu – Bi. Ruth Zaipuna akiwa ameambatana na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Bw. Filbert Mponzi pamoja na viongozi wengine wa Benki, wameshiriki kushuhudia uwasilishwaji wa Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali, Bungeni - Dodoma leo. Hotuba hii yenye mapendekezo ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2025/2026 imewasilishwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba. Jukumu letu kama Benki ni kuendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kuunga mkono juhudi za kukuza uchumi shirikishi na huduma jumuishi za kifedha kwa Watanzania. #NMBKaribuYako
