
Dimbani Konekti
206.5K subscribers
Verified ChannelAbout Dimbani Konekti
Kwa habari, uchambuzi na taarifa za kina za michezo na burudani kutoka kote duniani.
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

*Kwa kuangalia msimamo, kuna haja ya kujua matokeo yao?* ๐ Weka imoji hapa tujue mood yako๐


Nyota wa klabu ya Vipers kutoka nchini Uganda, Abubakar Lawal raia wa Nigeria amefariki dunia kwa ajali ya pikipiki (bodaboda) tukio hilo limetokea asubuhi ya leo akielekea mazoezini. Lawal si tu alikuwa mchezaji wa kutumainiwa bali pia alimiki historia nzuri hasa mioyoni mwa mashabiki wa Vipers ambao wataendelea kumkumbuka kwani aliwafungia bao la kwanza kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika, nyota huyo alijiunga na klabu hiyo msimu wa 2022/23 akitokea AS Kigali FC.


*Hasheem Imbwe atamba kuwa wakibebwa kama Simba SC na Yanga watakuwa mabingwa mara 10 mfululizo* ๐ Ingia https://youtu.be/P3j1VnCWO2Y?si=B5lNzmTKlwOZt-i0

*Ahmed Ally Kinyonge kawanyooshea mikono Azam* Ingia https://youtu.be/NALV7u3MXzU?si=mxwRzeUL_JfzfyLM

Pita kulia nipite kushoto tukutane kwa Mkapa, ndio leo ni Mzizima Derby mchezo utakaopigwa saa 1 usiku katika dimba la Benjamin Mkapa baina ya Simba SC dhidi ya Azam FC. Simba wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kupata ushindi ugenini Ruangwa dhidi ya Namungo, wakati Azam wakidondosha alama pale Sheikh Amri Abeid Arusha kwa Wagosi Wakaya Coastal Union. Azam wakiwa na alama 43 watajitutumua kupunguza wigo wa alama dhidi ya wapinzani wao Simba wenye alama 50. Vita ni Vita Mura.๐ฃ


Hii ndio orodha ya vinara wa Kutoa pasi za usaidizi wa goli/Assists katika Ligi Kuu ya Nbc ๐น๐ฟ 2024-25 hadi sasa: ๐น๐ฟ Feisal Salum: 1๏ธโฃ1๏ธโฃ ๐ฟ๐ผ Prince Dube: 7๏ธโฃ ๐ง๐ซ Aziz KI: 7๏ธโฃ ๐จ๐ฎ Jean Ahoua: 6๏ธโฃ ๐จ๐ฎ Pacรถme Zouzoua: 6๏ธโฃ


Timu ya Taifa ya Wanawake โTwiga Starsโ leo itashuka dimbani ugenini dhidi ya Equatorial Guinea majira ya saa 11 jioni, katika mchezo wa kuwania tiketi kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 zitakazofanyika Morocco. Huu utakuwa mchezo wa pili baada ya ule wa kwanza Stars ikiwa nyumbani Uwanja wa Azam Complex Chamazi, kushinda mabao 3-1 yaliyofungwa kipindi cha pili na Stumai Abdallah na Enekia Lunyamila waliongia wakitokea benchi na lile la tatu la Diana Msewa. Stars ikifuzu fainali hizo, itaungana na timu nyingine za taifa za Tanzania zilizofuzu kwenye mashindano makubwa ya Afrika, Taifa Stars iliyofuzu Afcon, 17 Serengeti Boys iliyofuzu Afcon U17 na Ngorongoro Heroes Afcon U20.


Ratiba michezo ya Raundi ya 22 Ligi Kuu NBC, kwa mechi mitatu kupigwa. 14:00 | Fountain Gate FC vs Tanzania Prisons Tanzanite Kwara - Manyara ๐๏ธ 16:15 | Singida Black Stars vs Mashujaa FC CCM Liti - Singida ๐๏ธ 19:00 | Kagera Sugar vs KMC FC Kaitaba Stadium - Kagera ๐๏ธ


Klabu ya Real Madrid wameendelea kuonesha nia ya kunasa saini ya mlinzi Jarrad Branthwaite, anayekipiga kunako klabu ya Everton lakini wanapata kigugumizi kutoka na dau la Muingereza huyo. Everton wanahitaji dau la pauni milioni 62 kwa ajili ya kumuuza beki huyo wa kati wa England mwenye umri wa miaka 22.


*Leo ๐ดSimba SC inashuka dimbani kucheza na โช๏ธAzam FC mchezo wa Ligi Kuu ya NBC. Nani kuibuka mshindi?*