Nukta Habari WhatsApp Channel

Nukta Habari

46 subscribers

About Nukta Habari

A product of Nukta Africa

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

Nukta Habari
Nukta Habari
6/9/2025, 2:26:20 PM

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linatarajiwa kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake, baada ya Bunge la Tanzania kupitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya NHC wa mwaka 2025 ikiwemo kuipa Bodi ya Wakurugenzi uwezo wa kuwekeza bila kuhitaji idhini ya Waziri wa Ardhi. Marekebisho hayo yanaifanya NHC kuwa na uhuru zaidi katika uwekezaji na utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Mamlaka na Majukumu ya Msajili wa Hazina, Sura ya 370 kuhusu uwekezaji wa mashirika ya umma https://nukta.co.tz/bunge-lapitisha-muswada-wa-sheria-ya-marekebisho-ya-nhc

Nukta Habari
Nukta Habari
6/9/2025, 2:24:48 PM

Kasi ya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Mei 2025 umeng’ang’ania katika kiwango cha asilimia 3.2 kama ilivyoripotiwa Aprili, 2025 ikichangiwa zaidi na kupungua kwa kasi ya bei za bidhaa zisizo za vyakula. Mfumuko wa bei ni kasi ya ongezeko la bei ya bidhaa na huduma nchini na kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imebainisha kuwa kusalia kwa kasi hiyo ya mfumuko wa bei kumechangiwa na kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa baadhi ya bidhaa za vyakula. https://nukta.co.tz/mfumuko-wa-bei-tanzania-wanasa-kiwango-cha-aprili-2025

Nukta Habari
Nukta Habari
6/11/2025, 3:43:14 PM

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara katika nchi za Msumbiji na Visiwa vya Komoro ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano wa kihistoria, kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na mataifa hayo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Juni 11, 2025 jijini Dodoma na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, Rais Samia amepokea mialiko rasmi kutoka kwa Marais wa nchi hizo ili awe mgeni katika maadhimisho muhimu ya kitaifa, yakiwemo ya miaka 50 ya uhuru wa Msumbiji. https://nukta.co.tz/rais-samia-kufanya-ziara-msumbiji-komoro

Nukta Habari
Nukta Habari
6/9/2025, 3:48:13 PM

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo saba kwa Jeshi la Polisi yanayolenga kuboresha utendaji kazi wa jeshi hilo ikiwemo kuzingatia maadili, kuongeza mapambano dhidi ya dawa za kulevya pamoja na kulinda amani wakati wa uchaguzi. Rais Samia aliyekuwa akihutubia katika sherehe za kuhitimisha mafunzo ya Maofisa na Wakaguzi wa Polisi leo Juni 9, 2025 katika viwanja vya vya Chuo cha Taaluma ya Polisi Jijini Dar es Salaam amewaambia wahitimu kuwa wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kusimamia viapo vyao. https://nukta.co.tz/maagizo-7-ya-rais-samia-kwa-jeshi-la-polisi

Nukta Habari
Nukta Habari
6/9/2025, 2:07:10 PM

https://nukta.co.tz/mfumuko-wa-bei-tanzania-wanasa-kiwango-cha-aprili-2025

Nukta Habari
Nukta Habari
6/10/2025, 4:53:32 PM

Viwango vya kubadili fedha za kigeni dhidi ya shilingi ya Tanzania

Post image
Image
Nukta Habari
Nukta Habari
6/12/2025, 6:33:27 AM

Tumia viwango hivi kubadili fedha za kigeni dhidi ya shilingi ya Tanzania

Post image
Image
Nukta Habari
Nukta Habari
6/12/2025, 6:32:18 AM

Kupitia Nukta TV YouTube fuatilia uwasilishaji wa Hali ya Uchumi mwaka 2024 pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Serikali kwa mwaka 2025/26 utakaowasilishwa na Waziri wa Mipango na Uwekezaji Prof Kitila Mkumbo. https://www.youtube.com/live/YXwrPYl0Dyc?si=IY6CCSCHG5kxX4DZ

Post image
Image
Nukta Habari
Nukta Habari
6/9/2025, 2:20:48 PM

https://nukta.co.tz/mfumuko-wa-bei-tanzania-wanasa-kiwango-cha-aprili-2025

Post image
Image
Nukta Habari
Nukta Habari
6/9/2025, 7:57:40 AM

Viwango vya kubadili fedha za kigeni dhidi ya Shilingi ya Tanzania vinavyotumika leo Juni 9, 2025 na benki za CRDB Bank Plc @nmbtanzania

Post image
Image
Link copied to clipboard!