
Kigoma Region Tanzania
1.2K subscribers
About Kigoma Region Tanzania
Jumuiya ya Watu wa Kigoma (Kigoma People's Community) Lengo kuu ni kuwaleta wanakigoma pamoja kama familia moja yenye lengo moja la kusaidia kuharakisha maendeleo ya Mkoa wetu wa Kigoma kuanzia mtu mmoja mmoja hadi makundi ya watu. Hii ni Jumuiya ambayo inawaleta watu wote pamoja bila kujali maeneo yao, kabila zao, dini zao, hali zao za kiuchumi wala utashi wao wa kisiasa. Mjumuiko huu unafanya kazi kwa lengo la kuleta Nguvu kwa pamoja katika kuendeleza na kuharakisha maendeleo ya Mkoa wa Kigoma. Jumuiya ina malengo mengi na mikakati mingi itakayo tuhusu sisi kama wanafamilia. Tutawajibika pia katika matukio ya kudhibiti ujinga, maradhi, umasikini, kuinua uchumi, Elimu, Vipaji, Fursa, Ajira, Kushiriki Habari na matukio, Haki na Usawa kwa watu wa mkoa wa Kigoma. Tunasimama kama kielelezo chema cha kuutangaza mkoa wetu ndani na nje ya mipaka ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jumuiya ya Watu wa Kigoma inafanya kazi nchi nzima na inamuhusu Mwanakigoma yeyote yule popote pale alipo.
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

*PICHA: CHUO CHA UALIMU KABANGA* Chuo cha Ualimu Kabanga kilichopo Halmashauri ya Mji Kasulu ni miongoni mwa miradi mikubwa iliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita ili kuhakikisha watoa huduma ya Elimu (Walimu) wanapatiwa Mazingira bora na yenye miundombinu wezeshi ili kuwaimarisha katika nyanja za ujifunzaji na ufundishaji katika kufanikisha utoaji na upatikanaji wa Huduma bora ya Elimu Awali, Msingi na Sekondari sambamba na Elimu Maalum. https://whatsapp.com/channel/0029VabqKek7oQhlIA20XA2P


*KUADIMIKA KWA DAGAA ZIWA TANYIKA HIZI NI MOJA YA SABABU* Iko hivi, kikawaida Dagaa hushuka chini kutoka gezini kwa kufukuzwa na migebuka, migebuka hula dagaa, sasa dagaa hujinusuru kutokana na migebuka kwa kukimbilia maji ya chini kutoka gezini, hivyo na kuleta giza na ndipo wavuvi sasa huwavua dagaa kwa urahisi wanaposhuka chini. Ni toleo la kukimbizwa na migebuka na huu ndio mfumo wao wa maisha. Uvuvi haramu wa Filimayaa hufuata migebuka huko huko gezini na kuivua, tena huvua migebuka wadogo (Nyamnyam) kiasi kwamba dagaa hawashuki chini na hivyo dagaa kuanza kuadimika. Wakongomani wanapanda gezini kufuata migebuka kwa Filimayaa, Watanzania wanapanda gezini kufuata migebuka kwa Filimayaa, Warundi wanapanda gezini kufuata migebuka kwa filimayaa, Wazambia nao wanapanda gezini kufuata migebuka kwa filimayaa. Ziwa lipo katika hatari kubwa kwa ustawi wa mwambao huu. Filimayaa ni nyavu maalumu kwa kuvulia migebuka, wavu mmoja wa Filimaya unaweza kuchukua mita 70-100. Kila mtumbwi wa filimaya unakuwa na nyavu 4 na zaidi, sawa na mita 400 ukubwa wa viwanja vinne vya mipira. Eneo la Nanga kijiji cha Sibwesa peke yake kuna zaidi ya mitumbwi 500 ya Filimayaa. Uvuvi huu haramu hufanyika nyakati za usiku, wao hutupa nyavu zote kwenye maji kuanzia majira ya jioni hadi asubuhi kisha hutandua na kuchukua migebuka iliyonasa nyavuni. Kwanini samaki wa Filimayaa hawana ladha na huwahi kuharibika? ni kwasababu samaki ananasa nyavuni jioni saa mbili usiku anafia hapo anabakia anaelea kwenye maji, inapofika asubuhi ndio hutolewa na kupelekwa sokoni, kwa hivyo wanawahi kuharibika kwasababu wanakaa sana kwenye maji. Kigoma tulikuwa hatuna tabia ya kuweka samaki kwenye barafu, ila ulipokuja uvuvi huu samaki nyingi zinawekwa kwenye barafu kuepuka uharibifu mkubwa. Dagaa wamebaki wanapatikana maeneo yale yenye hifadhi za Taifa kwasababu hakuna shughuli za uvuvi ndipo dagaa hukimbilia eneo hilo la hifadhi, hifadhi ya gombe, mahale, Lake shore lodge, Nsumbu n.k Karibuni wamiliki wa vyombo vya Filimayaa tujadili swala hili kwa pamoja. https://whatsapp.com/channel/0029VabqKek7oQhlIA20XA2P


*BAADHI YA SAMAKI NA MAJINA YAO Ziwa Tanganyika* Mgebuka/Mkeke Nonzi Sangara Ndubu Manje Singa Malala Ndomondomo Kuhe Shanana Vijhole Kingongo Ntanga Nyika Msiha Mbanga Ngege Mbirigi Mbaraga Kakamsi Kavungwe Visarallah Kungura Nungi Mange Ndafa Somba Kikwera Kimizi Rumbu Mgara Mshekele Mrombo Vindulwa -Mzungu wachini -Kikarakacha -Kihongo -Mlangala *#Utalii wa ndani* *#Ziwa Tanyanyika* *#Ziwa lapili kwakina Duniani* *#kigoma Tanzania*

*UMOJA WA VIJANA WAKIGOMA KARIAKOO MWAKA 1980 RAHA STREET* *#Upendo* *#Nidhamu* *Kuheshimiana* *#Hii ndio kigoma*

*MALENGO YETU KIGOMA COMMUNITY NA KIGOMA REGION TANZA* Hii ndio kazi inayotakiwa kuanza kuifanya *Jamii ya watu wakigoma* Mungu afanye wepesi tuzifikie Jamii Zetu na kuzisaidia. Nia tunayo,Ari Tunayo tunahitaji support kutoka kwa Jamii yetu. Watu wetu Wakigoma bado wanahitaji kushikwa mkono na kutatuliwa shida zao. *#Jukumu letu*

*USAFIRI NDANI YA MTO MALAGARASI -KIGOMA* *#UTALII WA NDANI* *#UTALII KIGOMA* https://whatsapp.com/channel/0029VabqKek7oQhlIA20XA2P

*HII NI KWA MATUMIZI YA MTU YEYOTE ANAETOKA KIGOMA* Kumbuka anuani hii unaweza kuitumia na wewe katika shughuli zako za kiofisi na mambo yako mengine binafsi yaliyo halali, usisumbuke anuani ya kutumia, ikiwa tu hauna anuani mkoani Kigoma basi tumia anuani ya Jumuiya. Muhimu kutoa taarifa. JUMUIYA YA WATU WA KIGOMA S.L.P 734 KIGOMA, TANZANIA. Wilaya ya Kigoma, Kata ya Kigoma Mjini, Mtaa wa Shede, Barabara ya Bangwe na Stanley, Nyumba Na: 02 Barua pepe: [email protected] Namba ya simu +255744753493 .... Au ... KIGOMA PEOPLE'S COMMUNITY P.O.BOX 734 KIGOMA, TANZANIA Kigoma District, Kigoma Town Ward, Shede Street, Bangwe and Stanley Road, House No: 02 Email Address: [email protected] Phone Number +255744753493

*WANAKIGOMA WALIOWAHII KUALIKWA /KUHOJIWA NA KUONESHA NJIA KUNAKO MAENDELEO YA MKOA WETU KUPITIA KADA MBALIMBALI KUPITIA WAO TUMEONA MABADILIKO MAKUBWA MKOANI KWETU* *TUNAOMBA KUWATAMBUA* *1-Hussein Kalyango:* Diwani kata ya Kigoma Manispaa ya Kigoma Ujiji 2015-2020. *2-Mr Kagoma:* Kiongozi wa Tembo FC Kibondo Kigoma. *3-Husna Sungura:* Kiongozi wa soka la Wanawake mkoani Kigoma *4-Ally Itembe* : Kiongozi wa soka mkoa wa Kigoma (General Coordinator wa TFF Kigoma) *5-Lulu Cement:* Kiongozi wa kurasa za Mashujaa FC *6-Chief LutaLosa Yemba:* Mgombea Urais Jamhuru ya Muungano wa Tanzania 2015 ADC *7-Dk Zimbwe Kauke* pharmacist (Dodoma Hospital) *8-Mh Hamisi Iddi mmasa* M/kiti Kijiji Cha Sunuka willaya ya UVINZA *Ccm*. *9-Mh Omari Gindi* mwekiti wa Chadema Wilaya kigoma mjini. *10-mwalim Banka the don* muonesha fursa Katavi. *11-Kolo Hamza malilo ll* Sultan wa wamanyema *12-Mbuya Ayoub kilima*. Makamu m/kiti chama Cha mpira wamiguu kigoma. *13-Hasan Hamis msimbwa* mfanyabiashara/Muonesha fursa na mshirika wachama Cha wafanyabiasha wamipakani.*Cross Border Traders Association CBTA* *14-Rashid Bakari Tanganyika* Meneja wa Taasisi ya *matwi Sports Academy* *15-Paul Wabike* Fursa za kibiashara Nchi za Ulaya. *16-Dr Mikota Karenga* (Masters Degree) Ufadhili wa Masomo Nchini Uturuki *17-Ernest Boniface Makulilo EBM*. Udhamini wa Elimu ya Juu Ughaibuni. *18-Jumbe Issa Jumbe* katibu wachama Cha mpira wamiguu Wilaya ya Kasulu. *19-Said Msonga* Mchambuzi wa masuala ya kisiasa Ukanda wa Ulaya,Africa,Ulaya. *20-Mwalim Abuu Mvano* Afisa Uhamiaji mstaafu_kigoma. *21-Mh Shaabani Mambo* Mwanachama na Kiongozi wa ACT wazalendo_kigoma. --------- *Tunawashukuru sana na tuendelee Kushirikiana kwa Ajili ya maendeleo ya mkoa wetu Wakigoma* Wanakigoma mnakaribishwa ktk Mijadala mbalimbali ili kupanua fikra kwa Ajili ya maendeleo mkoani kwetu kigoma.

*KIGOMA BROTHERS* *LEO KTK HISTORY* Hawa ni vijana watanashati kutoka mkoani kigoma Ujiji Enzi hizo. Wazee wetu wameanza Harakati za kuupambania mkoa wetu Kigoma kabla ya uhuru na kusaidia Jamii Yao ya kigoma. Wanayohistori yenye kutukuka ndani ya mkoa wetu Umoja wao huo wa *KIGOMA BROTHERS* waliuunda Mahususwi kwa Ajili ya kuwasaidia ndugu zao Wakigoma waliopo Dar es salaam wanapofikwa na matatizo,magonjwa n.k..wao hujitoa na kuwasaidia bila ya Ujira wowote. Hii ilionesha kujali na kuthamini Jamii Yao ya watu Wakigoma na kujitoa kwa Moyo wao mkunjufu. Nahii waliifanya kwa bila Kubagua huyu anatoka Wilaya ipi ktk mkoa Wakigoma. Walikua na Upendo sana wazee wetu Enzi hizo. Kwa kuthamini mchango wao ,utu na undugu kwa watu Wakigoma na tawataja kwa majina Yao kama Ilivyoripotiwa kutoka kwenye makitaba ya Jamii ya watu Wakigoma kutoka mji mkongwe wa UJIJI. *Kuanzia Kushoto waliosimama* Marehem Mzee Aman Fukuza. Marehem Mzee Idd Ally Lubumba. Marehem Mzee Abdulbari, na Marehem Mzee Ally Juma Lhey. *Walioketi kutoka Kushoto* Marehem Mzee Rajab Kitete Marehem Mzee Omar Fukuza Marehem Mzee Abdallah Fundi Mwamba na Marehem Mzee Juma Rangam. Mungu awalipe Kila lakheri na awaondolee Adhabu ya akaburi. Picha hii imepigwa Tarehe 05/04/1951 wazee wetu wamenyuka pamba safi na watanashati haswaa *#kigoma ya Upendo* *#Kigoma yetu* Tuwape Mauwa Yao 🌹🌹🌹🌹🌹 https://whatsapp.com/channel/0029VabqKek7oQhlIA20XA2P