
TRT Afrika Swahili
11.8K subscribers
Verified ChannelAbout TRT Afrika Swahili
*Afrika kama ilivyo* 🌐 https://www.trtafrika.com/sw Tiktok ▪️ https://www.tiktok.com/@trtafrikasw Facebook ▪️ https://www.facebook.com/trtafrikaSW Youtube ▪️ https://www.youtube.com/@trtafrikasw X ▪️ https://x.com/trtafrikaSW Instagram ▪️ https://www.instagram.com/trtafrikasw
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Ni jiji gani la kwanza kufikia idadi ya watu milioni moja Afrika Mashariki?

“Sitaondoka hapa isipokuwa ni kuelekea kufanya hajji” Hujaji mmoja kutoka Libya aliyeachwa na ndege amekuwa gumzo baada ya ndege hiyo iliyomuacha kushindwa kuendelea na safari hadi walipomkubalia kupanda ndege nao kuelekea Saudia https://trt.global/afrika-swahili/article/2e3d0e768ef1

Kimnyole Arap Turukat alikuwa ni kiongozi wa nne wa kiroho katika jamii ya Wanandi nchini Kenya, mwanzoni mwa miaka ya 1800. Alisifika sana kwa tabiri zake, ambazo kwa kiasi kikubwa zilibadilisha maisha ya Wanandi kutoka bonde la ufa nchini Kenya. https://youtu.be/ejpv5aMpWec

Ni jiji gani la kwanza kufikia idadi ya watu milioni moja Afrika Mashariki?

Sikiliza muhtasari wetu wa habari ya siku ya 19 Mei 2025 🎧 Sikiliza hapa: https://www.trt.global/afrika-swahili/audio/d191d5fcfec3


Mwenyekiti wa chama cha upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu, mapema hii leo amefikishwa katika Mahakama ya Mkazi ya Kisutu iliyopo jijini Dar es Salaam. Lissu anakabiliwa na mashtaka kadhaa ikiwemo la uhaini. Viongozi mbalimbali, kutoka chama chake cha Chadema, pamoja na baadhi ya wanaharakati kutoka nchini Kenya wamehudhuria kesi hiyo. Awali kumekuwa na taarifa za kuzuiwa kuingia nchini Tanzania kwa baadhi ya wanasheria na wanaharakati kutoka Kenya na hatimae kurudishwa nchini mwao. Aliyekuwa waziri wa katiba Kenya Martha Karua pamoja na mawakili wengine walizuiliwa kuingia Tanzania siku ya Jumapili. Jumatatu Jaji Mstaafu wa Kenya Willy Mutunga na wanaharakati wengine walirudishwa nyumbani. Lakini jaji mwingine mstaafu wa Kenya David Maraga aliruhusiwa kuhudhuria kesi ya Tundu Lissu jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, serikali ya Tanzania, bado haijatoa ufafanuzi wa sakata hilo.


Rais wa Kenya, William Ruto kwa mara nyingine amewakashifu wakosoaji wake hasa wa kisiasa, wanaopinga uongozi wake. Akitoa mfano, alisema wapinzani hao hawana mawazo mbadala ya kukuza uchumi wa nchi.


🇷🇼 Rwanda imelalamika vikali kuhusu vikwazo vilivyotangazwa na serikali ya Uingereza katika kukabiliana na mzozo wa mashariki mwa DRC. Uingereza inaishtumu Rwanda kuunga mkono kikundi chenye silaha cha M23 nchini DRC, ambacho tangu Januari 2025 kimefanya mashambulizi mengine mashariki mwa nchi.

🇨🇩 Zaidi ya watu 7,000 wameuawa mashariki mwa DRC tangu Januari huku waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wakiteka miji na maeneo kadhaa. Kambi 90 zimeharibiwa na watu wengine 450,000 kuhama makazi yao, Waziri Mkuu wa DRC Judith Suminwa ameitaja hali hiyo kuwa “ya kutisha,” akihimiza hatua za kimataifa kukomesha vurugu na kutekeleza azimio la Umoja wa Mataifa.


Mwishoni mwa juma aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga, ameshindwa katika uchaguzi wa Uenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika nchini Ethiopia. Hii imempa yeye fursa ya kurudi nyumbani, ambapo anasema kuna “majukumu muhimu” yanayomsubiri. Hata hivyo, hii si mara ya kwanza kwa mwanasiasa huyu mzoefu kushindwa katika uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa. Katika safari yake ya kisiasa ya zaidi ya miongo minne, ameshindwa mara tano alipojaribu kugombea urais nchini Kenya, lakini mara nyingi amepata njia ya kupenya mwanasiasa mwenye ushawishi na huwa na mchango mkubwa hata akiwa upande wa upinzani. Tunaangazia vipindi alivyokuwa kwenye uchaguzi na kupata matokeo ambayo hayakumridhisha.
