MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚 WhatsApp Channel

MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚

105 subscribers

About MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚

🤏"Tafuteni elimu, mkishindwa kutafuta elimu basi wapendeni wenye elimu, mkishindwa kuwapenda basi msiwachukie"👌

Similar Channels

Swipe to see more

Posts

MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 10:33:37 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 3:50:18 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 10:33:39 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 10:33:38 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/23/2025, 4:19:36 PM

8. Hii ni maalum kwa wenye kuwapeleka watu Hijja na 'Umra: *wasionekane vituko zaidi ya wale mahujaji wao:* Hawa viongozi wa taasisi wawe kama mfuaji/msafishaji wa nguo au chombo - mikono yake isafike zaidi. Isiwe Hajj (aliyekwenda Hijja) tena ndio kwanza awamu ya kwanza akawa na uafadhali kwenye utekelezaji wa ibada kuliko yeye, au akageuka kituko kwenye ibada hizo - ima kwa kupuuzia au kuleta mchezo na masihara kwa vile kwake limekuwa jambo la mazoea. Tubadilikeni waja wa Allaah - hasa tunapokuwepo kwenye ibada hizo na pale tunaporudi tuwe mifano mizuri kwa wengine tusiangalie maslahi yetu tu, bali tuangalie zaidi maslahi ya ibada hii. 9. *Tumuombe Allaah tawfiiq:* Allaah atuwafikishe kuweza kuitekeleza ibada hii - huku tukiamini kuwa sio mali zetu wala afya zetu kuweza kuitekeleza ibada hii bali ni kwa Tawfiiq yake Allaah - hivyo mtu asifanye mchezo katika ibada yake hii. Pia tuwaombee wale ambao Allaah hajawawafikisha kuitekeleza hii ibada - awatie nguvu nao waitekeleza kwa kutafuta radhi zake Allaah subhaana. Baaraka llaahu fiikum

MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 10:33:39 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 10:33:41 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/24/2025, 10:33:40 PM
Post image
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/23/2025, 9:49:34 PM

SHAIRI: SEMA NAYE Mtunzi: Tulaybu 1.Naukunjua mkeka, njoo tushauriane Dada yangu pia kaka, nasaha tuambiane Kamwe tusifuge taka, vema tunasihiane Mapema useme naye, singoje muda upite 2.Sema na wako mtoto, mapema angali chini Ni baridi au joto, mfunze awe makini Awe Kurwa au Doto, mpe maneno laini Mapema useme naye, singoje muda upite 3.Mpe elimu kijana, elimu ya maadili Ya leo sio ya jana, azitulize akili Sema bila kuyabana, yasimzonge maswali Mapema useme naye, singoje muda upite 4.Watoto lao hitaji, wayafikie malengo Hivyo kwenye ukuaji, usiwaachie pengo Wasiwe wazururaji, maisha ya songombingo Mapema useme naye, singoje muda upite 5.Hali imeshachafuka, kwa wakike na kiume Watoto wahitajika, maadili wayasome Sio usiku kuruka, mithili ya paka chume Mpema useme naye, singoje muda upite 6.Mjengee marafiki, wema wasio waovu Sio wale wanafiki, mwanao mpe makavu Muonye kama hataki, kwa upole utulivu Mapema useme naye, singoje muda upite 7.Ukae naye karibu, mfanye wako swahiba Umzoeshe vitabu, hwena akaleta toba Atazijua adhabu, maovu akiyabeba Mapema useme naye, singoje muda upite _____________________ Sat, 24 May 2025 Tulaybu ✍️ 0714388284

Post image
👍 1
Image
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
MEFTAHUL 'ULUUM 📚🔑📚
5/23/2025, 4:11:26 PM

*MUKHTASAR WA IBADA YA HIJJA NA 'UMRAH:* ________________ ●Maandalizi ya safari ya Hijja No. 0️⃣4️⃣ 5. *Achague mali ya halali:* chumo lake liwe la halali na kuihudumia familia yake kwalo kwa kiasi ambacho Allaah amemkunjulia. Asiwe ni mwenye azma ya kwenda kufanya Hijja au 'Umra lakini chumo lake na matumizi yake ni katika yale yasiyomridhisha Allaah. 6. *Kuusia kunako kumcha Allaah _subhaanahu wata'alaa _ kwa siri na kwa dhahiri.* Muislamu yampasa aiusie nafsi yake na watu wake daima kwa kumcha Allaah na kufanya maamrisho na kuachana na makatazo katika maasi, hasa hasa wewe uliyeikusudia ibada hii. Kwani Taqwa hiyo ndiyo zawadi bora zaidi. 7. *Uwajibu wa kufahamu matendo ya Hijja na 'Umrah:* mtu anatakiwa ajifunze ibada hii kabla ya kuitekeleza ili ajue usahihi wa utekelezwaji wake kama alivyoelekeza Mtume _swalla llaahu 'alayhi wasallama_ Na ikiwa kuna jambo linamtatiza au halifahamu afanye pupa ya kuwauliza wanachuoni. ...... inaendelea

Post image
Image
Link copied to clipboard!