
JamiiCheck
83.3K subscribers
Verified ChannelAbout JamiiCheck
A citizen-centered approach in countering Misinformation and Disinformation Online and Offline by JamiiForums
Similar Channels
Swipe to see more
Posts

Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Kimataifa la Nishati (IEA) za mwaka 2022, Afrika Kusini inaongoza kwa uzalishaji wa umeme barani Afrika, ikichangia 25.9% ya uzalishaji wote, sawa na Gigawatt 234,850. Nchi zinazofuata ni Misri, Algeria, Morocco, Nigeria, Libya, Ghana, Tunisia, Msumbiji, na Zambia, huku Tanzania ikishika nafasi ya 18. Aidha, kwa mujibu wa Ceicdata, kufikia Novemba 2024, Afrika Kusini ilizalisha umeme wa Gigawatt 216,310, sawa na wastani wa Gigawatt 19,664.55 kwa mwezi. Soma https://jamii.app/UzalishajiUmemeAfrika


Ifahamu Teknolojia ya Deepfake, namna inavyoweza kutumika katika kupotosha taarifa pamoja na mbinu zitakazokuwezesha kugundua Video iliyotengenezwa kwa kutumia Teknolojia hii Soma https://jamii.app/DeepfakeVideos

Ikiwa umepata Taarifa na unaitilia mashaka Usahihi wake, ilete JamiiCheck ili kupata majibu ya Uhakika. Tembelea JamiiCheck.com, weka Taarifa unayotaka Kuhakikiwa, na utapata majibu punde baada ya Uhakiki. Usikubali Kupotoshwa.


Kumekuwapo na Taarifa inayodaiwa kuchapishwa na Mwanahalisi Digital kuwa Tundu Lissu alisema ni mfaidika nambari moja wa maridhiano, hivyo ni muhimu yakawepo. Ufuatiliaji uliofanywa na JamiiCheck kwa kutumia maneno muhimu (KeyWord Search) umebaini kuwa Taarifa hiyo imetengenezwa, Si ya Kweli na haijachapishwa na Mwanahalisi Digital. Hata hivyo Chapisho hilo limebainika kuwa na mapungufu kadhaa, ikiwemo ukosefu wa alama ya mistari inayozunguka upande wa juu na mpangilio wa maandishi kwenye kichwa cha habari, tofauti na machapisho rasmi ya chombo hicho. Soma https://jamii.app/LissuMaridhiano


Kumekuwapo na Taarifa inayosambaa mtandaoni ikidai kuwa Februari 16, 2025, Millard Ayo alichapisha Taarifa kuwa Tundu Lissu alisema "No Reforms, No Election" haiwezi kufanikiwa. Ufuatiliaji wa kimtandao wa JamiiCheck kwa kutumia maneno muhimu (KeyWord Search) umebaini kuwa Taarifa hiyo Si ya Kweli, na haijachapishwa na Millard Ayo. Vilevile, Lissu hakutoa kauli hiyo. Aidha, chapisho linalodaiwa kuwa la Maria Sarungi na kutumiwa katika Taarifa hiyo Potoshi, Si la Kweli, kwani hakuwahi kulichapisha kwenye akaunti yake ya X. Soma https://jamii.app/LissuNoReformsNoElection


Wakati wa matukio makubwa, Upotoshaji pia huibuka kwa kiwango kikubwa. Mathalani wakati wa uchaguzi, kipindi cha usajili wa wachezaji ama mlipuko wa magonjwa. Thibitisha Taarifa mara kwa mara ili uweze kufanya maamuzi sahihi kutokana na kile ulichokisikia ama kukiona. Tembelea jukwaa la JamiiCheck.com kujifunza mbinu za Uthibitishaji wa Taarifa na kuona Taarifa zilizofanyiwa Uhakiki.


Tafiti mbalimbali zimebainisha kuwa nyama ya samaki aina ya papa ina kiwango kikubwa cha kemikali ya Zebaki (Mercury) yenye madhara makubwa kwa afya ya Binadamu. Kemikali nyingine ni Lead, Arsenic, na Urea. Hali hii inatokana na papa kuwa samaki mkubwa miongoni mwa viumbe wa mwisho katika Ikolojia ya bahari, na huishi kwa muda mrefu, hivyo huhifadhi kemikali hiyo mwilini mwake. Kwa mujibu wa tovuti ya Koiko Conservation International, ulaji wa nyama ya papa iliyo na kemikali hiyo unaweza kusababisha athari kwenye moyo, ini, figo, mapafu, na hata kusababisha kifo. Soma https://jamii.app/NyamaYaSamakiPapa


Shughuli ya kuhakiki taarifa na maudhui yanayopatikana ndani nje na ndani ya mtandao inaendelea ndani ya Jukwaa la JamiiCheck.com Karibu Jukwaani uwasilishe taarifa unayotaka ihakikiwe na ushiriki katika mchakato wa kuhakiki taarifa nyingine ili kupata uhalisia wake
